Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nichukue nafasi fupi sana kuchangia katika Wizara hii, lakini awali ya yote niwapongeze sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri na timu yake ya wataalam. Nawapongeza kwa kazi kubwa waliyofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala ambalo nitachangia kwa kiasi kikubwa sana ni matumizi mbadala ya mkaa pamoja na kuni. Kama ambavyo wameeleza wenzetu katika taarifa hii, mkakati waliouweka ni pamoja na kuonyesha kwamba matumizi ya mkaa pamoja na kuni yanapungua kwa kiwango kikubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo mkakati mkubwa na wenye dhamana kubwa ya kuhakikisha kwamba mkakati wa kuni na mkaa unaisha na kwamba sasa tunatumia nishati mbadala ni Wizara yetu ya Nishati na Madini, kwa hiyo nitajielekeza kwenye hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni tuna mpango wa kimataifa wa matumizi endelevu unaotaka kuhakikisha kuwa matumizi ya mkaa pamoja na kuni yatakomea ifikapo mwaka 2030.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hayo, kwanza kabisa nitumie nafasi hii kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge na wananchi kwa ujumla kwamba matumizi ya mkaa katika nchi zinazoendelea hadi sasa yanafikia asilimia 90 ya nishati ya umeme duniani. Hiyo ni takwimu ya Benki ya Dunia. Lakini pamoja na hayo bado kwa nchi zetu zinazoendelea hasa zilizoko chini ya Kusini mwa Afrika, pamoja na maendeleo ya nchi za Afrika tani milioni 2.3 kwa nishati tunayotumia inatokana na kuni pamoja na mkaa. Kwa hiyo, ni changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama Serikali, mpango madhubuti uliopo ni kwamba, moja, sisi ni wanachama wa kimataifa wa matumizi mbadala ya nishati ya kuni pamoja na mkaa. Mkakati madhubuti ambao Serikali tumechukua, napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, ni kwamba sasa Shirika letu la TPDC kuanzia mwaka 2013/2014 lilianza rasmi kujenga miundombinu ya matumizi ya gesi kuanzia mijini mpaka vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa hatua ya kwanza, tumeanza na Dar es Salaam. Mwaka 2014/2015 tumeshaunganisha wateja 70 ambao tumewaunganishia miundombinu ya gesi katika maeneo ya Mikocheni. Kwa hiyo, ni hatua kubwa, lakini hatua ya pili tumepeleka matumizi hayo hayo ya gesi kwenye magari yetu. Hadi sasa tunapozungumza magari takriban 60 yanatumia gesi, hiyo ni hatua ya kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hatua ya pili ni kupeleka miundombinu ya matumizi ya gesi, na hii gesi ninayoizungumzia ni ya aina hii ya mathane, si ile gesi ambayo tumeizoea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kuna taarifa yetu itakuja hapo baadaye tutaeleza kwa upana zaidi; lakini kwa ufupi tu niseme kwamba kuanzia mwaka 2017/2018 tutaunganisha matumizi ya gesi katika Mikoa ya Mtwara na Lindi pamoja maeneo yote ya Dar es Salaam yakiwemo maeneo ya Mbagala, Kurasini, Buguruni na maeneo mengine ya jiji ya Dar es Salaam. Tunatarajia wananchi 30,000 tunawaunganishia gesi ili matumizi makubwa ya mkaa na kuni yapungue. Asilimia 70 ya mkaa unaotumika hapa nchini unaingia Dar es Salaam, kwa hiyo tukishaunganisha gesi kwa wananchi wa Dar es Salaam tutapunguza kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira, hiyo ni hatua ya kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili, kwa sababu muda ni mfupi sana, inahusu usambazaji wa umeme mijini na vijijini. Kama ambavyo mnajua tunapeleka umeme katika mikoa yote katika miji yote na vitongoji vyetu. Tuna mpango wa kendeleza umeme mijini, na mpango huu unaanza mwaka 2017/2018 kwa maeneo ya mjiniā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.