Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na umuhimu wa Wizara hii ya Maliasili na Utalii ambayo inachangia pato kubwa kwa Taifa letu, kuna kila sababu ya kubadilisha utaratibu wa kuendesha Wizara hii ili kuongeza idadi ya watalii nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubadilisha aina ya matangazo kutokana na hali ya ushindani ni mkubwa sana, ni vyema Serikali ikabadilisha utaratibu wa matangazo kwa vivutio vilivyopo nchini kwa kutumia njia kama shuleni, ngazi ya msingi, sekondari na vyuo vikuu na vyuo vya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miundombinu ili kupata watalii wengi nchini kwa kutengeneza miundombinu ambayo itakuwa rafiki kwa watalii wanaokuja nchini ili kuongeza idadi ya watalii na kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya wananchi kulingana na migogoro ambayo inaendelea nchini katika maeneo mbalimbali ikiwemo Simanjiro ambao umechukua muda mrefu sana kupeleka mifugo na wananchi kuuawa, ni vyema migogoro hii ikamalizwa kwa wakati na bila kuathiri haki ya binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka ya hifadhi ichunguzwe upya kwani idadi ya watu imeongezeka lakini maeneo ya hifadhi pamoja na mapori tengefu wakati ardhi ni ile ile. Hivyo, nashauri Serikali kupitia upya mipaka hiyo ya maeneo ya hifadhi ili kuwatendea haki wananchi wanaoishi karibu na hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na uzoefu na matatizo mengi yanayotokea katika maeneo ya hifadhaji ili utekelezaji wa yale waliyokubaliana yafikie malengo, suala la bajeti kufika kwa wakati kulingana na umuhimu wa Wizara hii ambayo ni miongoni mwa sekta muhimu za kiuchumi katika nchi yetu, ni vyema bajeti ikatolewa kama ilivyotengwa na kupitishwa na Bunge na iende kwa wakati.

Suala la kushirikiana na Wizara nyingine ambayo ni Wizara ya Ardhi, Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Kilimo ili kuweza kuwa na mkakati wa kudumu wa kumaliza changamoto zinazowakabili wananchi na watalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, manyanyaso kwa wananchi wanaopita katika hifadhi kulingana na hali iliyopo katika maeneo mbalimbali wanatakiwa kupewa elimu na siyo maamuzi na hatua kali zinazochukuliwa kwa mifugo na wananchi wetu.