Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara ijitazame kuchachua utalii katika maeneo yafuatayo:-

(i) Festival Tourism: Nchi lazima ijipange vyema kuanzisha matamasha mapya na kuimarisha yaliyopo. Nionavyo kama Taifa tutimize na ku-advertise Busara Festival na Zanzibar Film Festival, kwa sababu ya effect yake, tunaweza kuwa promoted katika kiwango cha Taifa. Ni kosa kutotangaza as part of National Tourism Campaign.

(ii) Songkran Festival ya Thailand ambayo ni ya siku tatu huingiza US Dollar 428.08 million. Afrika Kusini 35 percent ya utalii wake ni matamasha ya utamaduni. Tuwe na matamasha ya sanaa na mengine.

(iii) Nyingine ni Conference Tourism ambayo inatarajiwa kuipa Rwanda US Dollar 76 million mwaka huu na kupandisha utalii kutoka US Dollar 1.2 million kwa 2014 hadi US Dollar 1.3 million hapo mwaka 2015; na mapato kutoka US Dollar 318 million to US Dollar 400 million kwa kipindi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema sana kwa kuwa Dar es Salaam imepumua kuwa Capital City, sasa tukielekeza jiji hilo kuwa hospitality and commercial city na conference tourism ipigwe jeki kubwa kuifanyia matangazo. Tuhimize uwekezaji wa Multipurpose Convention Centers na hii itaendana vizuri na ujio wa uwanja wa ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, water sports ni muhimu pia.