Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Lwanfi Game Reserve iko Nkasi Kusini, hatujawahi kupata mchango wowote katika shughuli zozote za kijamii licha ya ukweli kuwa vijiji kama nane vimepakana na mbuga hii. Vijiji hivi ni Kasapa, Kiing’ombe, Mlambo, Kilambo, Ngundwe, Mlalambo, Kizumbi, Nkata, Namansi na vinginevyo kote huko tuna shida za kujenga miundombinu ya huduma za jamii ikiwemo ujenzi wa madarasa, zahanati, nyumba za walimu na shida ya maji tunaambulia vipigo vya mbwa mwizi pale ambapo mwananchi anapokamatwa na mbao moja tu. Tunaamini tuna mchango katika uhifadhi wa Lwanfi Game Reserve.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ukatili uliopita kiasi, licha ya umuhimu wa maliasili zetu kulindwa na askari wanyamapori lakini sheria hazifuatwi. Askari hawa huchukua sheria mkononi kwa kufanya matendo mabaya ikiwepo kuua, kutesa, kupiga sana na kadhalika. Jambo hili si la kistaarabu, tujaribu mara zote kufuata sheria labda kama mazingira yanahatarisha usalama wa wahifadhi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa misitu ya TFS; mamlaka hii kama imezinduka toka kusikojulikana, wameweka mipaka kwenye vijiji vyetu hadi ndani ya vijiji na kufanya vijiji vingine ambavyo vipo miaka mingi kisheria kuonekana havina ardhi kabisa. Maeneo yaliyokuwa yanalimwa na wananchi yametwaliwa na kukosa mahali pa kulima, wananchi wanalima, mnafyeka mazao. Kijiji cha Kasapa, Msitu wa Kalambo ni mfano unaothibitisha hali hii ambayo ni ukatili. Wananchi hutengeneza Serikali, mnawaadhibu namna hii, haikubaliki hata kidogo. Kamati ya kutathmini migogoro ije Nkasi tafadhali.