Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Katavi ni muhimu sana, inatakiwa kuwekewa mkakati wa kuboresha miundombinu kwani barabara ni chache. Pia hakuna sehemu za huduma kwa watalii kama simu, hoteli za hadhi ya nyota tano, barabara za ndani na visima vya upepo kukabiliana na ukame.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuendeleza ujirani mwema (corporate social responsibility), hifadhi za Taifa husaidia kero mbalimbali. Hivyo basi, Hifadhi ya Katavi ina mpango wa kuchimba visima vitatu vya maji ambapo wananchi wanatakiwa kuchangia 30% ya gharama. Tunaomba Serikali ibebe mzigo/gharama zote za mradi ili kumsaidia mkulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania Tourism Board inahitaji fedha za kutosha ili kuweza kufanya kazi ya kutangaza utalii wa aina zote uliopo katika nchi yetu. Serikali lazima ihakikishe kuwa inatoa pesa kama sera ilivyo ambapo 3% ya mapato ya TANAPA na Mamlaka ya Ngorongoro yawe yanawasilishwa ipasavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma za utalii. Tanzania imekuwa na kiwango cha chini cha huduma katika utalii kutokana na kutokuwa na package nzuri kulingana na uwezo wa watu mbalimbali. Hivyo, TANAPA na Serikali ni muhimu kuhakikisha kuwa watoa huduma wanakuwa na elimu na uwezo wa kutosha pia kuwe na standard zinazofuatwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hifadhi za misitu; maeneo mengi ya Tanzania yamevamiwa na wafugaji hivyo tunahitaji Serikali kufanya mpango bora wa matumizi ya ardhi na kudhibiti uharibifu wa misitu. Hivyo, Serikali iangalie uwezekano wa kuongeza maeneo kiasi ili kuondoa migogoro. Mfano Halmashauri ya Nsimbo tunahitaji maeneo katika Kata za Ugala, Sitalike, Kange na Kapalala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.