Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara kwa utekelezaji wa majukumu yao kwa kiwango na cha kuridhisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali katika kukubali ombi la wakazi wa Wilaya ya Malinyi, Ulanga na Kilombero katika kufanya marekebisho ya mipaka ya Pori Tengefu la Kilombero kwa kushirikisha wananchi. Wakazi wa Wilaya hizo tatu tunafahamu umuhimu wa kuhifadhi Bonde la Kilombero na ardhi yake. Ushirikiano wanaopewa wananchi na wataalam wa wanyamapori katika kurekebisha mipaka sio rafiki kabisa kwani wanayokubaliana au kujadiliana na viongozi wa vijiji na kata au wananchi hayatekelezwi. Wananchi bado wana mahitaji ya kutengewa (kupewa) ardhi ya nyongeza kutokana na hali halisi ya kuongezeka kwa matumizi ya ardhi kwa kilimo, mifugo na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja kubwa ya wananchi hao ni kwamba ile ardhi ya buffer zone ni kubwa (pana sana) kwani kuna maeneo yana upana wa kilometa 8 -12. Ombi letu wakazi wa Malinyi, Ulanga na Kilombero upana wa eneo (ardhi) hiyo ya buffer zone ungepunguzwa iwe na upana wa angalau kilometa 1 au 2 tu kati ya ardhi za vijiji na kiini cha Pori Tengefu la Kilombero. Ardhi hiyo itakapoongezeka kwa wakazi itatupunguzia kwa kiasi kikubwa migogoro baina ya hifadhi, wafugaji na wakulima. Ahsante.