Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii


MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto za Mkoa wa Tabora ni kama zifuatazo:-

(i) Ukarabati wa jengo la utawala na maabara katika Chuo cha Nyuki Tabora ili kiwe cha kisasa;

(ii) OC kwenda kwa wakati, pia malipo ya wazabuni yaangaliwe;

(iii) Kutangaza Chuo cha Nyuki, nchini na nje ya nchi ili kupata wanafunzi wa kutosha; na

(iv) Kuanzisha mafunzo mbalimbali ya ufugaji nyuki kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kituo cha Tabora kwa miaka mingi hakifanyi kazi na kilianzishwa kwa ajili ya tafiti za nyuki, mazao ya nyuki na mizinga yenye tija na kusababisha wataalam na watumishi kukaa bila kazi. Kwani gari liliondolewa katika kituo hicho, pia mpaka computer zimetolewa, nini hatima ya Kituo hicho cha Utafiti Tabora?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Mheshimiwa Waziri afike Tabora kujionea haLi halisi na Mkurugenzi husika ili kutatua changamoto hizo. Nakushukuru.