Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dua William Nkurua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. WILLIAM D. NKURUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hoja iliyotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza Wizara kwa kuainisha mambo mengi kwa ufasaha, lakini changamoto kubwa ambayo naiona ni migogoro kati ya mipaka ya hifadhi na wananchi (vijiji). Naomba Serikali ishughulikie kwa umakini sana tatizo hili. Mfano, katika Wilaya ya Nanyumbu kuna mgogoro katika vijiji vya Marumba kwenye vitongoji vya Nambunda na Namaromba na kijiji cha Mbangara Mbuyuni, kitongoji cha Wanika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakazi hawa wamekuwepo hapo kabla ya uhuru wa nchi hii lakini wananchi wamekuja kujua kuwa vitongoji hivyo vipo ndani ya hifadhi baada ya muda mrefu sana, takribani kama mwaka 2014. Hali hii inafanya wananchi kuchukia Serikali wakiamini kuwa wanaonewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ikaone hali halisi ya vijiji hivyo na ikiwezekana tuwaache wananchi ili waendelee na kazi, kuwaondoa tutawapeleka wapi? Gharama za ujenzi wa nyumba na mali mbalimbali nani atalipa? Naomba sana Serikali itatue haraka tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja