Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepongeza wakati wa kuchangia moja kwa moja Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri sana kwa dhati bajeti ya kitengo cha utangazaji wa utalii wetu kupewa kipaumbele ndani ya utalii kwa kutangazwa mapema vivutio vyetu kwani kuchelewa kwetu kunapelekea nchi jirani na vivutio hivyo kuvitangaza ndani ya nchi zao kama Kenya - Mlima Kilimanjaro au Zambia - Kalambo Falls(Rukwa) ni hatari na kutupunguzia mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuweke timu maalum ya kufuatilia vivutio hapa nchini na kutimiza taratibu kwa uharaka na kuvitangaza kwa kwenda sambamba na utekelezaji wa kuweka mazingira rafiki ya kuwafikisha watalii kwenye maeneo hayo. Tunashukuru Mkoa wa Rukwa Serikali kulishughulikia eneo la Kalambo Falls kuweka miundombinu, kasi hiyo iongezeke kukamilisha zoezi tuanze kupokea mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii ni muhimu sana kutekelezwa kikamilifu na Wizara ya Fedha kwa maana ya Hazina hutoa fedha kwa kufuata maidhinisho ya Bunge kwa hii Wizara kwani ina mchango mkubwa na unaweza kuongeza Pato la Taifa ikiwa itasimamiwa ipasavyo kwa maslahi ya nchi. Penye rupia penyeza rupia. Mfano, mwaka 2016/2017 kuliidhinishwa fedha za miradi ya maendeleo shilingi bilioni mbili na zikatolewa shilingi milioni 156.6 sawa na asilimia nane kwa fedha za ndani na nje wakatoa asilimia 82. Hali hii tunahitaji mabadiliko makubwa kwani sisi ndiyo wenye uchungu na haya maendeleo, kilio na mwenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matarajio yetu sasa ni kwa Wizara hii pamoja na upana wake, lakini ina maslahi makubwa kwa nchi na maendeleo kwa watu wake, hivyo bajeti ya mwaka 2017/2018 ya shilingi bilioni 51.8 itatoka hata asilimia 75, kwani tunahitaji kwenda kwenye nchi ya viwanda na uchumi wa kiwango cha kati na mafanikio yake mengi ni ya muingiliano na Wizara kadhaa, hivyo ni mtambuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho tunaomba hizo changamoto zilizofuatiliwa na timu ya pamoja za Wizara husika, taarifa hiyo ikafanyiwe kazi kwa mujibu wa taratibu na hatua husika. Ikibidi hadi Bunge tuletewe ili tuweze kufanya marekebisho kwa lengo la kuondoa malalamiko ya wananchi wetu na haya matope tunayopakana viongozi wa kisiasa na Kiserikali.

Mheshimwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.