Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri katika Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ni Mkoa wa Mwanza pamoja na kuwa makazi ya makabila zaidi ya manne, lakini Wasukuma ni wengi zaidi. Kuna utamaduni wa Kisukuma ambao umejengeka na kuhifadhiwa kwa njia ya ngoma na vitendea kazi vilivyokuwa vinatumika enzi za mababu zaidi sana historia ya uchifu kwa koo tofauti za Wasukuma umehifadhiwa vizuri.

Aidha, namna ya maisha waliyoishi na kuweza kudumisha amani ya maeneo yao lakini pia Kituo cha Bujora kimetunza kumbukumbu zote vema ambapo watalii wanaweza kutembea na kujifunza mengi. Rai yangu naomba Kituo cha Bujora kiingizwe katika maeneo ya vivutio vya utalii nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Victoria mbali na kuwa ziwa la pili kwa ukubwa duniani bado halijatangazwa vema, tunaweza kutangaza kivutio hiki kwa kuwekeza katika michezo ya ziwani kwa kuweka sports boats (speed boats) ambapo watalii wanaweza kushiriki kikamilifu. Aidha, wanaweza kufanya uvuvi (sport fishing) ambapo Ziwa Victoria ni tulivu, uvuvi wa aina hiyo ya utalii unaweza kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa uwanja wa ndege wa Mwanza upo katika upanuzi, bado watalii wanaweza kutumia uwanja huo kwenda Serengeti ambapo ni karibu zaidi tofauti na KIA ambako ndiko watalii wengi wanapitia.