Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, hongereni sana kwa kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu. Niwaombe mnisaidie kutatua migogoro ya maeneo yaliyohifadhiwa na jamii (WMA) ya Kimbanda, Kisungura na Mbarangandu dhidi ya wananchi walioyatoa maeneo hayo. Wananchi hao walitegemea mipaka ya WMA hizo ingepitiwa upya baada ya miaka kumi, kama walivyoahidiwa lakini inaonekana hakuna mpango wowote wa kupitia upya mipaka hiyo. Wananchi wameongezeka na wanahitaji maeneo zaidi kwa shughuli za kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba mridhie kuachia eneo linalogombaniwa kati ya Chuo chenu cha Likuyu Sekamaganga (Chuo cha Mafunzo ya Uhifadhi), hususan eneo ambalo halitumiwi na chuo hicho na limevamiwa na wakulima wakazi wa kijiji cha Kikuyu Sekamaganga. Eneo husika lilikuwa ni sehemu ya eneo la kijiji hicho na lilichukuliwa bila ya kulipiwa fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri aliyetembelea kijiji cha Likuyu Mandela kilichokumbwa na uharibifu wa mashamba uliofanywa na tembo ambapo baadhi ya wanakijiji hao kupoteza maisha kwa kuvamiwa na tembo hao. Naomba ahadi ya kulipa kifuta machozi na kipangusa jasho kwa waliouawa na tembo na walioliwa mazao yao na tembo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono kwa asilimia mia moja na nawataka utekelezaji mwema.