Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake kwa kazi nzuri wanazozifanya licha ya changamoto kubwa na nyingi zilizopo kwenye Wizara yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa heshima na taadhima Mheshimiwa Waziri apokee ushauri wangu kuhusu suala la kuwapa offer madaktari na timu yote ya madaktari hao kutoka Marekani ambao walifanya kazi kubwa kuwasaidia watoto wetu wa Kitanzania katika ajali iliyohusisha wanafunzi, walimu na dereva wa shule ya Lucky Vincent. Mheshimiwa Waziri, madaktari hawa walikuwa wamekuja Tanzania kwenye programu tofauti lakini wakiwa nchini waliona nia ya kwenda kutembelea vivutio vyetu ambapo walikutana na ajali hiyo eneo la Karatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, timu hii ilifanya kazi kubwa ya kuwasitiri watoto wetu ambao walifariki lakini waliendelea pia kuwasaidia waliojeruhiwa kwa kuwapeleka nchini Marekani kwa ajili ya matibabu. Huu ni moyo wa kipekee, kwani ilibidi wakatishe safari yao kutokana na tukio hilo. Naiomba Wizara licha ya ukweli kwamba madaktari hawa wana uwezo, lakini sisi kama Watanzania tuna njia nyingi za kuwashukuru kutokana na kitendo hicho, na kwa kuwa walionesha nia ya kutaka kwenda kwenye vivutio vyetu naona itakuwa ni jambo jema kama tukitambua mchango wao kwa kuwapa offer hiyo ya kuja bure kwenye vivutio vyetu popote watakapotaka kutembelea. Kama ikikupendeza basi tuwape offer ya muda mrefu ili waweze kujipanga na kuamua siku watakazotaka wao wenyewe.

Mheshimiwa Waziri, hiyo itasaidia kuonesha shukrani yetu lakini pia itasaidia kuendelea kutangaza utalii wetu hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.