Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia kuhusu fidia kwa wananchi. Katika maeneo mbalimbali ya nchi ambapo Hifadhi za Taifa zimepakana na vijiji ambavyo wananchi wanaendesha shughuli za kilimo kumekuwa na changamoto za wanayama kuharibu mazao ya wananchi na wananchi hawapewi fidia kutokana na uharibifu huo. Kilio hiki cha wananchi kimekuwa cha muda mrefu na wakati mwingine hata kama fidia inatolewa kwa kuchelewa sana na kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi. Hivyo basi naishauri Serikali ifanye yafuatayo:-

(a) Kulipa fidia kwa wakati; na

(b) Malipo ya fidia yalipwe na mamlaka husika ambapo uharibifu umetokea kwani kwa kufanya malipo ya fidia kuwa central kwa maana ya kulipwa na Wizara imekuwa na usumbufu mkubwa na kuchelewesha malipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya vijiji na hifadhi za wanyamapori; migogoro ya wananchi na mipaka au hifadhi za wanyamapori imekuwa ya muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi, matokeo yake Serikali imekuwa ikikimbilia kuunda tume ya kufuatilia migogoro bila mafanikio. Nashauri ije na mkakati wa namna gani inamaliza migogoro hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ya misitu, natambua umuhimu wa misitu na tunaunga mkono juhudi na jitihada za kulinda misitu. Miongoni mwa mazao ya misitu ni mkaa ambayo ni nishati muhimu sana kwa wananchi kwa ajili ya matumizi ya kupikia. Wizara imetoa katazo kuwa mkaa usitoke nje ya Wilaya. Katazo hili limekuja bila kuwepo na nishati mbadala kwa wananchi hao. Miji ambayo haina sasa watakosa nishati ya mkaa na wananchi hawawezi kumudu gharama za gesi. Nashauri Serikali ifute katazo hili huku tukiwandaa wananchi kutumia nishati mbadala ambayo wataiweza na kuimudu.