Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Wakurugenzi wote na watendaji wote wanaohusika katika Wizara hii na sekta zote husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri/Naibu Waziri watakapokuja kutoa ufafanuzi, wanijulishe:-

(i) Wananchi wanaozunguka Mlima Kilimanjaro wanafaidikaje na mlima huo?

(ii) Ni lini elimu ya utunzaji wa mazingira itatolewa kwa wananchi hao, hususani wanawake na vijana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tembo wanaogopa sana nyuki, je, Serikali iko tayari kuwagawia mizinga ya nyuki wananchi wanaoishi maeneo yanayovamiwa na tembo ili kuwazuia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza zijengwe hosteli za bei nafuu kwenye mbuga za wanyama ili wananchi wa kawaida na wanafunzi wapate fursa ya kutembelea vivutio hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono asilimia mia moja.