Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri na Wizara kwa ujumla katika utekelezaji wa kazi za kuendeleza utalii hapa nchini Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni/ushauri; Wizara iendelee na kazi ya kuibua vyanzo vipya vya utalii na kuvitangaza duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Tanzania Forest Fund (TFF), Kamati iliyoundwa kuangalia jinsi ya kutoa fedha za utafiti wa kuendeleza misitu Tanzania, uhifadhi wa misitu na viumbe wadogo wadogo kuna malalamiko kwamba wanaopewa fedha hizo baadhi yao hawakidhi vigezo na baadhi hawajishughulishi na shughuli hizo kabisa. Nashauri ufuatiliaji wa karibu juu ya fedha hizo za Serikali zilizotolewa kama zimetumika zilivyokusudiwa. Kabla ya kutolewa fedha hizo ukaguzi ufanyike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nawatakia utekelezaji mwema wa majukumu yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja.