Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kuhusu utalii katika Jimbo la Rungwe. Tuna utalii katika Wilaya ya Rungwe ambao Serikali haijaweka mkazo katika uendeshaji wake na kuisaidia Serikali kuongeza mapato. Vivutio hivyo ni Daraja la Mungu na Lake Ngozi, vivutio hivi havina miundombinu ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kutangaza utalii nje ya nchi. Serikali iongeze pesa katika Wizara hii ili tuweze kujitangaza na kupata wageni wengi hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Kitulo haitatunzwa na Serikali kwa kupeleka pesa kidogo hivyo nashauri pesa zitengwe za kutosha kuweza kuitunza hifadhi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, misitu yetu, tunaomba Serikali itoe vibali kwa wazawa ili kuweza kuuza nje ya nchi miti na mazao yake na hivyo kuweza kuongeza kipato cha mwananchi mmoja mmoja na hatimaye wa Taifa.