Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa namna ya pekee kwa kweli niwape hongera sana Waziri wa Maliasili na Naibu wake, lakini pia na watendaji wote ambao kwa kweli wamefika mahali wamesaidia sana ujangili kushuka kwa kiwango kikubwa, hongereni sana kwa kupunguza ujangili katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo mambo mawili tu na ningeomba niyaseme kama ifuatavyo; kwanza ningependa kuzungumzia suala la msitu wa Taifa wa Makere Kusuni maarufu kama Kagera Nkanda. Msitu huu una ukubwa wa hekta 97,000 na msitu huu Waziri unanisikia msitu huu ulikuwa gazetted mwaka 1954 wakati eneo lile lilikuwa halina watu kwa kweli, sasa maeneo haya watu wameongezeka vijiji vimeongezeka na sasa watu wanasumbuliwa kujua mipaka halisi ya eneo lile na maeneo ya vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba sana Mheshimiwa Waziri na timu yako hasa wenzako wa TFS na juzi nilipata bahati kuzungumza hata na Dkt. Silayo kuhusu jambo hili, kwamba ni wakati umefika mkaweke mipaka upya, mka-re-map eneo lile kwa sababu watu wameongezeka na kama alivyosema jana Profesa Tibaijuka hapa jamani mazingira yamebadilika huwezi kuwa na mipaka ya 1954 leo ni miaka 60 ukasema mambo yatabaki yale yale, hawa wananchi wameongezeka na lazima utaingia kwenye maeneo kufanya shughuli zao za kujitafutia kipato na uchumi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri hili jambo tumelisema na ilishakuja Tume yako kule Kasulu tukalizungumza sana jambo hili, ningeomba sana suala la Kagera Nkanda lifikie mwisho na kwa kweli wananchi waweze kupata maeneo kwa ajili ya shughuli za kilimo.

Pia niseme kwamba popote itakavyokuwa juzi Mkurugenzi wa Wanyamapori alikuwa anatupa habari ya genesis ya biblia, lakini tukubaliane pia kwamba hakuna mahali popote kwenye biblia pamesemwa kwamba sasa viumbe hivi vya wanyamapori na misitu vitakuwa badala ya binadamu, la hasha! Lazima binadamu awe mbele kwa sababu wameumbwa na Mwenyezi Mungu kuweza kutumia rasilimali hizi.

Suala la Kagera Nkanda Mheshimiwa Waziri ninaomba na wenzako wa TFS lifike mwisho, mka-re-map mipaka ile, sisi hatuna shida na uhifadhi, lakini mka-re-map mipaka ile ili watu waweze sasa kupata maeneo ambayo wanaweza kuyatumia kwa kilimo na ninasema tena mwaka 1954 lile eneo lilikuwa halina watu kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa niliseme ni suala la la eneo oevu la Malagarasi, maarufu kama Malagarasi wetland. Eneo hili liko kwenye uhifadhi wa dunia chini ya UNESCO, chini ya Ramsar site, eneo hili linaharibika.

Mheshimiwa Waziri wale ng’ombe mliowafukuza kule Geita, ng’ombe waliotoka Burigi wamehamia kwenye chepechepe ya Malagarasi, sasa unataka tupoteze Mto Malagarasi? Kwetu watu wa Kigoma na watu hata Geita wenyewe, Malagarasi ni ikolojia ambayo ni muhimu sana kwa maisha ya watu wetu naomba sana maadam hii wetland ya Malagarasi, eneo oevu ama chepechepe la Malagarasi lipo chini ya Ramsar site, chini ya uhifadhi ya dunia, kwa nini lisilindwe kwa nguvu zote, kwa nguvu ya pamoja kati ya UNESCO, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara yako, maeneo haya tunayaacha yanaharibika na baadaye athari zake ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupotea kwa wetland ya Malagarasi maana yake ni kupotea kwa Ziwa Tanganyika, kupotea kwa Ziwa Tanganyika unajua madhara yake itakuwa ni makubwa sana. Hivyo nilikuwa naomba sana maeneo ambayo yametengwa, maeneo ambayo yametangazwa kidunia nina hakika, Wizara na Serikali mnaweza ku-join hands na watu wa UNESCO maeneo haya yakalindwa ili yaweze kuendelea kuwepokwa sababu binadamu lazima pia waendelee kuwepo.

Mwenyekiti baada ya kusema hayo mawili muhimu niliyokuwa nayo naomba niseme jambo moja la mbuga la Mahale na Gombe National Parks, hizi ni mbuga mpya, hizi ni mbuga virgin kabisa, nafikiri kupitia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii. Ahsante.