Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nilitaka kuchangia maeneo manne, lakini matatu nimeyaleta kwa njia ya maandishi ambayo ni kuhusu conference tourism, festival tourism na water sports tourism ambayo bado nchi hii haijatilia mkazo na haijawekeza vya kutosha. Lakini eneo ambalo nitalizungumza kwa urefu kidogo na ambalo nina interest lakini ninauzoefu nalo ni sports tourism ambayo hivi sasa inaambiwa ni the still sleeping giant, hii inafaida kubwa duniani na ikitumika vizuri inaweza kusaidia Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa globally sports tourism inatengeneza karibu 90.9 trillion dollars kwa mwaka mpaka 2017. Lakini kutoka 2015 ilikuwa 46.5 trillion dollars kwa hivyo ni biashara kubwa duniani lakini Tanzania bado hatujaitumia vizuri. Lakini hata katika individual sport kwa mfano golf, golf ni biashara kubwa na Kenya wanazungusha a lot of money kwa sababu wamewekeza katika golf. Wana viwanja vyenye kutosha yale mashimo yanayotakiwa vitano ambavyo karibu 35 percent ya watalii wanaokwenda Kenya ni wale ambao wanakwenda kwa ajili ya golf. Halikadhalika na Afrika Kusini nao wamewekeza katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwa ujumla golf ni biashara kubwa duniani na wanaongoza duniani ni Ireland ambao wanatengeneza wageni kiasi 165,000 kila mwaka wanatembelea Ireland kwa ajili ya issue ya golf wakati sisi hatujaitumia golf kama mchezo ambao unatusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata kwenye riadha mimi ningetarajia watu wa utalii wangehimiza sana marathon zote ambazo Tanzania wangejitokeza wakazidhamini na wakasimamia, lakini pia wakazikuza. Kuna mchezo kama cycling ambao tuna maeneo ambao unaweza ukatengeneza pengine Dar es Salaam to Tanga tunaona ile Paris mashindano ya baiskeli yanaisaidia sana na yanaitangaza sana nchi ile, Arabuni wanafanya mashindano ya baiskeli lakini sisi bado hatujaanza kutumia michezo katika hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muhimu ni kwenye individual sports ni rahisi kuwekeza. Kwa mfano Watanzania wote sasa hivi wanajivunia Simbu, Simbu lakini kumbe taasisi za kitaliii zingeweza kutengeneza Simbu wengine kumi kwa sababu kuwekeza katika individual sports ni rahisi kuliko kuwekeza katika team sport. Kwa hiyo, mimi ningewashauri watu wa utalii wawekeze kwa mtu mmoja/mmoja wamdhamini mtu mmoja/mmoja tunaweza tukatengeneza watu hasa watu ambao wanakimbia kwenye marathon.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingini ni kwenye mpira wa miguu na hili tayari naelezea interest yangu nimeshawaandikia TANAPA ni decleare interst nimeshawandikia TANAPA programu ya namna ya kuweza kuileta timu kutoka Ulaya kuja kucheza Tanzania. Eneo la pre-season ambao ni kuelekea kwenye ligu kuu za nchi za Ulaya timu nyingi za Ulaya zinapenda kwenda nje ya nchi zikafanye mazoezi na sisi Tanzania hatujaitumia. Nimekuwa nikisikia kwamba Everton inaweza ikaja hapa lakini tunaweza tukaleta Everton na tukaleta na timu nyingine na nyingine. Kwa hiyo, pia ningetaka watu wa utalii wawekeze katika eneo hili kwa sababu inakuwa na fedha nyingi. Wenzetu Thailand, Singapore na wengine huwa wanafanya kila mwaka na tayari kama nilivyosema nimewapelekea TANAPA pengine wataona kama inafaa wataitumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna timu za ndani hapa tumezoea kuwekeza kwenye Yanga na Simba. Lakini Yanga na Simba at the end of day sio kwa maana ya kuingia watu uwanjani, lakini kwa maana ya kuonekana wanaonekana timu zingine zinaonekana kama timu nyingine katika television hasa Azam Tv ambayo kusema kweli sasa hivi ni globally brand, inafika mbali.

Kwa hiyo, watu wa utalii silazima wawekeze kwenye Yanga na Simba ambao wanapata wafadhili mbalimbali NMB, Sport Pesa na wengine lakini pia wanaweza wakajitokeza kwa mfano timu ambayo najaribu kui-promote timu ya Lipuli au timu nyingine zilizopanda daraja wakawavisha jezi zao wakazi-brand matangazo ya utalii at the end of the day kwa maana ya kuonekana wanaonekana ninety minuties sawasawa wanavyoonekana Yanga na Simba na kwa hiyo, wataonekana dunia nzima. Kwa hiyo, ningependa hiyo pia mlifanyie kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najiuliza tuliambiwa hapa kwamba tulikuwa tunatangaza kwenye klabu za timu za nje hasa ilikuwa Sunderland lakini suala hili liliulizwa mwaka jana halikupata majibu ya kutosha. Na kwa hiyo bado kuna haja ya kutumia matangazo ya nje lakini very strategical, mwaka jana nilishauri kuhusu Samatta siju limefikia wapi lakiniā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante,