Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizari ya Maji na Umwagiliaji

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizari ya Maji na Umwagiliaji

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza na mimi nianze kuunga mkono suala la kuongeza bajeti ya Wizara ya Maji. Tatizo, Hazina hawatoi fedha zote za Miradi ya Maendeleo. Hilo ndiyo tatizo! La pili, Mji wa Mpwapwa, Mheshimiwa Waziri anaufahamu, amekaa Mkoa wa Dodoma miaka mingi akiwa Wizara ya Ujenzi. Vyanzo vya Maji vya Mji wa Mpwapwa tangu Ukoloni ni vile vile. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri atume watafiti wakafanye utafiti wa vyanzo vingine vya maji ili kuongeza huduma ya maji katika Mji wa Mpwapwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni uchimbaji wa mabwawa katika vijiji. Waliahidi kuchimba mabwawa Vijiji vya Chunyu na Msagali ili kusaidia bonde la Msagali ambapo kuna kilimo cha umwagiliaji. La tatu, kuna visima vitatu vya maji vimechimbwa katika Kijiji cha Iyoma, Bumila pamoja na Mima. Tayari maji yamepatikana, lakini visima vile havijawekwa pampu, mabomba, matenki ya maji ili kusambaza maji. Naomba Wizara ya Maji na TAMISEMI wasaidiane pampu ziwekwe, maji yasambazwe ili wananchi waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.