Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. USSI SALUM PONDEZA AMJAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kushiriki katika kuchangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nijielekeze kwenye maeneo ya Jimbo langu la Chumbuni ambalo lina matatizo ya Kituo cha Polisi ambayo bajeti ya mwaka jana niliyasema na kikaahidiwa kuwa nitapatiwa matengezo na nitapatiwa kituo katika Jimbo langu la Chumbuni Zanzibar, mpaka sasa hivi sijapata. Nilikuwa na kituo kimoja tu kidogo ambacho mpaka sasa hivi nacho hakifai kinavuja, kazi hazifanyiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kubwa zaidi ambalo nataka kulisema hapa leo ni vitendea kazi vya Jeshi la Polisi hususan Zanzibar. Polisi wetu hawana vifaa vya kutendea kazi sana hasa hasa Jeshi letu la Traffic. Unakuta Jeshi la Traffic wanaongoza magari kwa kutumia simu zao za mkononi. Redio hawana, hata sectionnne hazifiki, vitendea kazi ambavyo ni muhimu. Tumeshuhudia Zanzibar mara mbili ama mara tatu Viongozi wetu Wakuu wa nchi, madereva wanaingilia misafara yao kutokana na kutokuwepo kwa taarifa ambazo zinakuwepo kabla,hii yote ni kutokana na ukosefu wa vifaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Jeshi la Polisi Zanzibar lina deni katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika vikosi vyake vya Jeshi la Kujenga Uchumi yaani JKU ni kitengo cha NIDA mamlaka ya Vitambulisho, wanadaiwa karibu milioni 172 ambazo hawajazilipa mpaka sasa hivi. Nataka kujua leo hapa lini watazilipa fedha hizi milioni 172 katika JKU ya Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho napenda ambacho napenda kushauri Jeshi letu la Polisi au Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, linaonaje likafikiria kuweka sheria hata wale ambao ni Makamishna wa Jeshi hili. Kwa mfumo uliopo nafahamu wapo Makamishna tisa, kuanzia Kamishna Kaniki, Kamishna Amdan, Kamishna Musa na wengine wapo tisa, wakistaafu anayefahamika kwa mafao ni IGP peke yake. Kwa nini, Jeshi la Polisi lisiwe na mfumo kama Jeshi la Wananchi Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.