Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Na mimi bila kupoteza muda nichukue fursa hii kukupongeza wewe kwakuniruhusu kuchangia. Vilevile nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa muda mfupi kuwa Waziri katika Wizara mbili tofauti, hii ni kutokana na utendaji wake na umakini wake Mheshimiwa Waziri. Nikupongeze vilevile kwa timu ya Singida United kupanda daraja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimpongeze Kamishna Hamdani Omar Makame kwa kutuongoza vizuri Zanzibar katika kipindi chake na nimtakie kila la kheri na mapumziko mema ya kikazi. Nitakuwa sijamfanyia haki Kamishna Johari Masoud Sururu waImmigration Zanzibar kwa kazi anayoifanya Zanzibar, amekuwa makini katika utendaji wake bila ya kujali mvua, jua, usiku, mchana anapiga kazi, nimpongeze sana Kamishna Sururu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nitakuwa sijamfanyia haki Kamishna Musa Ali wa Zanzibar, kwa kujenga vituo vingi Zanzibar vya polisi zikiwemo nyumba. Amejenga nyumba na vituo vya Polisi Paje katika Jimbo langu ninakotokea.Vilevile amejenga vituo cha polisi karibu saba kikiwemo cha Jambiani, Nungwi, Bumbwini, Kiboje, Meli Nne, Fumba, Jozani na Pemba – Chokocho. Mheshimiwa IGP huyu mtu nafikiri ni hazina kubwa sana unisikilize kwa makini Mheshimiwa IGP, amefanya kazi vizuri sana na kubwa zaidi kujenga Kituo cha Afya Ziwani katika Makao Makuu ya Polisi, kituo cha kileo kabisa, huyu ni mtendaji kazi kupita kiasi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waziri hapa unisikilize kwa makini vinginevyo shilingi nitaizuia. Kuna mjenzi nimeshakwambia mara mbili/mara tatu, amejenga nyumba na Kituo cha Madungu anadai shilingi milioni 220, leo mwaka wa tano anahangaika,mpaka akapata maradhi anafanya mazoezi bila kutaka kupata ngazi kwenda na kushuka.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili nitakuwa mkaidi sana kama hujamlipa haki yake na Mwenyezi Mungu kamjalia kapata maradhi ya mitihani sasa hivi. Mtu anadai shilingi milioni 220; ameshajenga vituo, leo miaka mitano na baya zaidi hata kwenda kukaguliwa hazijaenda kukaguliwa, hilo ni jambo la kusikitisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri na IGP naomba mnisikilize, kumekuwa na kilio cha Wabunge humu ndani kunyanyaswa na wanaambiwa baada ya miaka mitatu muda wao wa Ubunge umekwisha, kuna Mbunge wa Ulanga yumo ndani humu, anaonesha kitambulisho kwa traffic anaambiwa wewe baada ya miaka mitatu Ubunge wako unaisha, siyo kauli nzuri hiyo.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili tunalipigia kelele katika vikao vyetu siku zote. Traffic wamekuwa wameshika mpini, Mbunge hana thamani mbele ya traffic. Leo Mbunge wa Ulanga yule anaambiwa baada ya miaka mitatu na kitambulisho anatoa, hatuwezi kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu hali za uchakavu wa nyumba, Mheshimiwa Waziri ulikuwemo Ziwani umeona askari wetu wanaishi vipi, mchana haendi kujisaidia, anakaa mtu upande huo huko anamwambia nitizamie mtu anakuja huko, ili apate kwenda chooni! Hali hairidhishi, mazingira siyo mazuri wanayofanya askari, vitendea kazi havipo, tunafanya nini? Hali ya Ziwani ndiyo Makao Makuu ya Polisi hairidhishi.(Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile askari wanakaa muda mrefu kupandishwa vyeo, anafika miaka 15 mpaka mtu anakaribia kustaafu hajapanda cheo! Hii siyo halali.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya vituo vya polisi vimekuwa vichakavu sana, ulikaja Pemba, pia wale wanaojenga mbona hamuwalipi?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo nichangie kuhusu mahabusu.Polisi wanapata shida wanatoa pesa zao mfukoni kuwahudumia mahabusu.Pia hali ya bajeti Zanzibar kupiga doria, umekuwa mtihani vilevile mafuta.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Sitaunga hoja mkono mpaka jamaa apate haki yake.