Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu pekee kwa sababu ni dakika tano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muongeaji anasema mwanadamu uvumilivu unapomuishia anakuwa ni afadhali mnyama kuliko mwanadamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatukumuacha Lipumba na vibaraka wake na wanaomtumia kwa sababu

tunamuogopa, hapana. Tulimuacha kwa sababu Watanzania na dunia ijue ujinga wao na hao wanaomtumia kufanya ujinga ule. Watanzania waelewe ujinga wa Lipumba na hao wanaomtumia kudhihirisha ujinga wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyama vya siasa vipo kwa mujibu wa sheria. Vyama vya siasa waasisi wa kuleta vyama hivi vya siasa mmojawapo ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mnamuita Baba wa Taifa na sisi tunakubali ni Baba wa Taifa, hawezi kutokea mjanja akamuona Baba wa Taifa aliyekubali vyama vingi vije nchi hii ni mjinga yeye ndiyo mwerevu, huyo ni zumbukuku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme wazi kwamba mgogoro unaoendelea ndani ya Chama cha Wananchi (CUF)kwa kupandikizwa na watu tunaowajua, akiwemo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania, Mheshimiwa Hamad Yussuf Masauni. Mheshimiwa Waziri umesema maneno makubwa sana nakuheshimu na katika Mawaziri kwenye Bunge hili ninaowaheshimu ni Mheshimiwa Mwigulu, lakini msaidizi wako hafai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, umesema Mheshimiwa Waziri hakuna ushirika wowote wa waovu utakaoweza kuishinda haki, nakubaliana na wewe sana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri Masauni umekuwa ukifanya mambo kadhaa kwa kushirikiana na hao mnaoona wanaweza kuiuwa CUF, lakini nikuambie hukuijua ilivyozaliwa na hutoishuhudia ikifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kuna matukio 13 ya utekwaji wanayofanyiwa watu wa CUF na bado watu wa CUF tumeendelea kudumisha amani na kuvumilia. Hivi niambieni yule mwendawazimu aliyetumwa na hawa akina Maftaha juzi, akapigwa pale, kama siyo uvumilivu na ukomavu wa watu wetu, angekuwa hai leo? Angekuwa hai leo kama si ustaarabu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wetu, chama chetu, viongozi wetu wameendelea kuilinda amani na kuhakikisha damu haimwagiki kama anavyotaka Mheshimiwa Masauni imwagike ili apate sababu ya kufuta chama chetu. (Makofi)

Mheshimiwa Hamad Masauni juzi uliratibu kikao cha kuhakikisha Tanga Mwenyekiti wetu hafanyi kikao, wewe kwa kushirikiana na Mheshimiwa Maftaha pamoja na mungiki wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumevumilia vyakutosha, hatumuogopi Lipumbana ninakuambieni sasa tunamnyoosha Lipumba na watu wake…

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwezo wa kumnyoosha tunao, nia ya kumnyosha tunayo na sababu ya kumnyosha tunayo.(Makofi)

Uvumilivu umetuishia, na ninakuambia hawa mungiki kwetu hawajai kwenye mkono mmoja.

Hawa ni wadogo sana, Chama cha Wananchi ni kikubwa sana ndani ya nchi hii, tunawaambia ifike mwisho na wakome, tupo tayari kwa lolote, lakini tutamnyoosha Lipumba na watu wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala la mrundikano wa mahabusu mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imezungumzwa sana kuhusu mrundikano wa mahabusu ndani ya magereza yetu. Hivi karibuni tunakwenda kwenye mfungo wa Ramadhani ilhali Masheikh wa Uamsho bado wakiwa gerezani wanaendelea kukaa bila kufikishwa mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, mungiki tutawanyoosha.