Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nimesoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri vizuri, ninapenda kusema si ajabu Waziri mwenyewe akawa chanzo cha matatizo ya askari wa Jeshi la Polisi. Hili nazungumza wazi kwa sababu kuna matukio ambayo yametokea polisi wakiwa wanatimiza wajibu wao, baadaye wanatengua walichokiandika wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili nazungumza sana kutokana na mgogoro ulioandaliwa na chama fulani ndani ya CUF. Tarehe 16 Novemba, 2016, nikiwa na Wabunge wenzangu wa CUF ambao ni Wajumbe wa Baraza kuu la Uongozi, tuliokwenda Newala kwa kibali cha polisi kwamba tunaruhusiwa kufanya mkutano wa ndani. Asubuhi tuko kwenye mkutano wa ndani, ghafla askari polisi wanakuja


na defender na washawasha wanakuja kutuondoa kwenye mkutano wa ndani, eti kuna mtu mwingine amewaambia kwamba haturuhusiwi kuendelea kufanya mkutano wa ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati sisi haturuhusiwi kufanya mkutano wa ndani ni siku tano nyuma Ibrahimu Lipumba aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF alifanya mkutano na wakamlinda. Tarehe 19 tulienda Mtwara…

TAARIFA...

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei hiyo taarifa, pia Kiti chako kisiyumbe. Kuna watu wameomba taarifa hapa umewakatalia mara kadhaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa mnaowabeba, ndiyo pamoja na hawa wengine hawa. Tarehe 19 Novemba Katibu Mkuu wa Chama changu cha CUF alikwenda Mtwara, anapaswa kufanya kikao cha ndani, tumelipia ukumbi na kila kitu, mwisho wa siku tunaambiwa haturuhusiwi kufanya kikao cha ndani.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukampigia Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, tukamwambia tatizo hili, lakini mwisho wa siku hatukupata maamuzi sahihi ya mambo haya. Mambo haya ya kihuni yanaendelea kufanywa na kundi hili la akina Lipumba na watu wake hawa akina Mheshimiwa Magdalena Sakaya, polisi wakiwa wanaendelea kuwalinda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF Taifa, Mheshimiwa Julius Mtatiro amekwenda Tanga katika vikao vya ndani, hakuna mgogoro, polisi wameendelea kuzuia wasifanye vikao vya ndani.

Polisi hawa pia wakati tuko mahakamani wanaona mtu anapigwa kwa kisu, yule aliyepiga mpaka leo hajakamatwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huko Mabibo Mwenyekiti wetu wa Wilaya ya Kinondoni, Juma Mkumbi, ameitisha kikao na waandishi wa habari, wameingia wavamizi na bastola, hawajakamatwa mpaka leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, matukio yote haya na Waziri ana barua ya chama ya kulalamika juu ya matukio haya ambalo Jeshi linaendelea kuwakumbatia hawa mungiki. Hata mkutano wa tarehe 21 Agosti, 2016, Lipumba kaingizwa kwenye mkutano na polisi kuvamia mkutano ambao mwenyewe Lipumba amekiri hakualikwa. Kama uliangalia kipindi kile cha 360 cha Redio Clouds, Lipumba mwenyewe anakubali hakualikwa, amevamia mkutano akiwa naOC- CID wa Magomeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo mnakaa hapa mnazungumza, nikuombe Mheshimiwa Waziri, ulitia nia kubwa ya kutaka nafasi kubwa mwaka juzi ya Urais wa nchi hii, si ajabu Mungu kwa makusudi kabisa aliona bado na ndiyo haya unayoyafanya. Kwa sababu haiwezekani, watu wanaofanya matukio wapo, tumesharipoti kesi nyingi, matukio anayoyafanya Lipumba anasindikizwa na polisi. Tumeomba juzi kwenda kufanya usafi Buguruni, Mbunge wa Temeke mmemzuia, Lipumba mlikuwa mnamlinda pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri dhamana uliyopewa ni dhamana kubwa sana. Mwanadamu kuna muda anavumilia na kuna muda uvumilivu pia unashindikana. Mimi nasema hawa mnaowatumia, mmemtumia Sakaya anakwenda kushtaki watu polisi anasema tunataka kumshughulikia, watu ambao hatukuwepo...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa muda wako umemalizika.