Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mungu kwa afya njema aliyonijalia. Nitumie fursa hii kuipongeza Wizara kwa hotuba nzuri yenye mipango yenye kuleta matumaini kwa wasanii, wanahabari na wanamichezo.

Mheshimiwa Spika, moja kwa moja nianze kuchangia hoja iliyopo mezani. Kumekuwa na changamoto kubwa ya watoto wa Kitanzania kutokua na ushiriki mkubwa katika michezo. Hivvyo, basi tumekuwa tukijenga Taifa lisilo na hamasa ya michezo. Hivyo basi, nipende kuishauri Serikali kufanya jitihada za kurudisha michezo mashuleni ambayo itaweka wanafunzi katika hali ya kuepuka hata vishawishi. Sambamba na hili, Serikali pia irudishe ushiriki wa wanafunzi katika sanaa na utamaduni kama hapo zamani.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la ukosefu wa timu za kushiriki katika michezo kama volleyball, handball, badminton, table tennis na kadhalika ambayo Tanzania kama Taifa tumekua tukijisahau na kuelekeza nguvu nyingi katika baadhi ya michezo kama mpira wa miguu. Naiomba Serikali iwezeshe ukuaji wa michezo ya aina yote kwa usawa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kituo cha makumbusho cha Bujora. Hiki ni kituo cha makumbusho ya kabila la Kisukuma kilichopo Mwanza, Wilaya ya Magu. Kituo hiki kimepoteza umaarufu wa hadhi yake hata kupelekea upungufu wa watalii wa nje na ndani kulingana na miaka ya nyuma. Bujora Sukuma Museum inahitaji fedha ili kuweza kuimarishwa na kukarabatiwa kurudi katika ubora wake.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi, naiomba Serikali kulisimamia suala hili kwa ukaribu ili kituo hicho kiimarike na kwa kufanya hivyo tutaongoza utalii ndani ya Mkoa wa Mwanza na kwa ujumla Serikali itapata kuongoza ukusanyaji kodi.

Mheshimiwa Spika, baada ya mchango wangu huu mfupi, naomba kuunga mkono hoja.