Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe na timu nzima waliofanikisha hotuba hii.

Mheshimiwa Spika, niipongeze timu yetu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 kwa mafanikio na heshima kubwa inayoiletea Tanzania. Niiombe Serikali bila kujali matokeo ya mashindano yatakayofanyika Gabon baada ya mwezi huu, Serikali isiwatupe vijana hawa, kwani wameonesha uwezo na vipaji vya hali ya juu, kutokana na umri wao kuwa mdogo tuwekeze zaidi kwao na naona akina Samatta wengi kutoka kwa vijana hawa.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF); ni ukweli usio na shaka hali katika shirikisho hili sio nzuri, migogoro na malalamiko ambayo kwa kiasi kikubwa tulishaanza kuisahau wakati wa uongozi uliopita chini ya Rais Leodgar Chills Tenga kwa sasa imerudi kwa kasi sana. Naomba sana Mheshimiwa Waziri asimamie vizuri shirikisho hili na kwa kuwa watafanya uchaguzi mwaka huu wapate viongozi wazuri ambao wataipeleka Tanzania mbali kupitia mchezo huu wa soka.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Natambua Wizara hii inawajibika kwenye Wizara hii kupitia maudhui na usajili wa vyombo vya habari. Tumeshuhudia magazeti na vipindi vya runinga vinavyoenda nje ya maadili, tumeshuhudia magazeti yakiandika habari za uongo na uzushi dhidi ya viongozi, Mheshimiwa Waziri mwenyewe ni muathirika wa jambo hili. Ushauri wangu, Serikali ichukue hatua kali ikiwa ni pamoja na kufungia maisha magazeti au Televisheni zinazothibitika kufanya vitendo hivi vya kuchafua majina ya watu.

Mheshimiwa Spika, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC); usikivu wa TBC Redio upo chini ya asilimia 25 kwa nchi nzima, niiombe Serikali iongeze bajeti ya TBC ili iweze kuwekeza katika mitambo na kuongeza usikivu hadi vijijini ambapo ndipo wananchi walipo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii na naunga mkono hoja.