Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza Serikali na Wizara kwa ujumla katika juhudi zake za kuendeleza michezo, sanaa na utamaduni nchini. Serikali iweke mkazo zaidi katika kuipa nguvu lugha ya Kiswahili kwa kutumia lugha hii katika shughuli na hafla mbalimbali za kitaifa na kimataifa ili lugha yetu hii iweze kuongeza idadi ya watumiaji na pia kuongeza soko la ajira kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, utamaduni; Serikali iendelee na juhudi za kutoa elimu kwa wananchi juu ya mila potofu zinazoathiri afya za wananchi. Serikali iendelee na juhudi za kutoa elimu kwa wananchi juu ya tamaduni zinazokandamiza wanawake, watoto na jamii kwa ujumla. Wasanii wapewe elimu ili wasiitumie sanaa kudhalilisha wanawake kwa mavazi yasiyoendana na maadili ya Mtanzania.

Mheshimiwa Spika, TBC iongezewe nguvu ya vitendea kazi, rasilimali fedha, watumishi wa kutosha ili redio na TV ziweze kusikika na kuonekana nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.