Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naunga mkono hoja, hata hivyo yapo mambo machache yanahitaji maboresho kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mchezo wa mpira wa miguu ndiyo mchezo unaopendwa sana duniani kote, uongozi wa TFF unasababisha matatizo makubwa kwa makundi mbalimbali ya wapenzi wa mpira wa miguu hususan pale wanaposhindwa kusimamia haki za vilabu vya mpira na wanachama wake kwa kupotosha maamuzi yanayolenga kufanya upendeleo, kunyima haki na kuonesha kuegemea upande fulani. Jambo hili ni aibu, tunahitaji viongozi walio juu ya ubinafsi na upendeleo wowote kwenye maamuzi yao.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni viwanja vya mpira wa miguu. Upo utaratibu wa TFF kutumia msaada wa FIFA unaotolewa kwa wanachama wake kuweka nyasi za bandia kwenye viwanja vinayoteuliwa. Ni busara kuweka utaratibu mzuri wa viwanja gani tunadhani vianze kuwekewa nyasi hizi kabla ya kufikiria labda viongozi wetu TFF wanapeleka nyasi bandia katika mikoa wanayotoka. Viwanja vya mpira vya Jamhuri Dodoma, Jamhuri Morogoro, Majimaji Songea vingestahili kuwekewa nyasi za bandia kwanza kuliko ilivyo sasa.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli tunahitaji viongozi wa TFF wasio na upendeleo wa ovyo ovyo. Nchi hii yetu wote, wote tunayo haki sawa, ni vema viongozi wawe watenda haki kwa wanaowaongoza. Kwenye mpira wa miguu TFF ni tatizo, wajirekebishe.