Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nichukue nafasi hii kuungana na wenzangu kuunga mkono bajeti ya Waziri Mkuu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mjadala ambao ulikuwa unaendelea humu ndani wako watu waliosema hakuna utawala bora, Rais anaingilia mihimili mingine, mimi niseme, hivi wewe ndiyo baba mwenye nyumba, mke uliyemuoa ana watoto amekuja nao...
MHE. DEO K. SANGA: ...amezaa na mtu mwingine na mtu mwingine, wewe ndiyo wa tatu…
MHE. DEO K. SANGA: Unasimamia watoto wa kwako na hawa, hivi hawa wengine wakiwa wezi huwezi kuwaambia acheni wizi?
MHE. DEO K. SANGA: Utaambiwa unaingilia? Ndugu zangu, kwa nini tunadhoofisha nguvu zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano?
Rais anafanya kazi nzuri sisi sote ni lazima tukubaliane kwamba Rais anafanya kazi nzuri. Mawaziri wake wanafanya kazi nzuri ni lazima tuwaunge mkono, tumeona kwa macho yetu wenyewe. Halafu tunakuja hapa tunasema anaingilia mhimili mwingine. Hivi mtu unakuwa mwizi asiseme kwamba jamani acheni wizi? Hawa Ofisi yako Waziri Mkuu na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli lazima waangaliwe vizuri watumbuliwe na wenyewe. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya CCM…
MHE DEO K. SANGA: Kila wakati mmesema Serikali hii hakuna chochote, hakuna kitu, sasa imeleta bajeti tangu mimi nimekuwa Mbunge hakuna bajeti nzuri na yenye mwelekeo mzuri kama hii, hii sasa imebaki ni ukombozi kwa Watanzania. Tuseme kweli jamani, tuwe wapenzi wa Mungu bajeti hii ina mwelekeo mzuri, inaonesha dira kwamba sasa angalau wananchi wetu matatizo mbalimbali yatapungua au yatakwisha kabisa katika miaka mitano, lazima tuipongeze Serikali ya CCM.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie sasa Jimbo langu la Makambako. Rais alipotembelea katika mji wetu wa Makambako aliahidi ahadi sita na moja kutatua tatizo la maji katika mji wa Makambako.
Pili ilikuwa ni lami kilometa sita katika mji wa Makambako; tatu ilikuwa ni fidia ya soko la kimataifa kulipwa kwa wananchi wa mji wa Makambako na nne ilikuwa ni vifaa vya upasuaji katika hospitali ya mji wa Makambako.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mji wa Makambako tumepata madaktari wazuri, tatizo kubwa tunalolipata gari letu la kubebea wagonjwa kila siku linapeleka mara tano, mara sita Wilayani Njombe kwa ajili ya upasuaji. Tuombe sana Serikali itupe vifaa vya upasuaji ili kupunguza gharama za kupeleka watu kule Njombe kila wakati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tano, ni kuimarisha uwanja wetu wa michezo na sita ilikuwa ni umeme vijijini. Ahadi hizi zote za Rais nimewapelekea Mawaziri wote wanaohusiana na Wizara hizi. Ombi langu wahakikishe wanazifanyia kazi ili ziendane na kasi ya Rais wa Awamu ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, pale Makambako upande wa Polisi ni Wilaya inayojitegemea Kipolisi, yupo OCD na kadhalika. Tuna eneo kubwa sana la kujenga nyumba za polisi hata nyumba moja ya polisi pale haijajengwa. Ombi langu tuhakikishe tunajipanga vizuri ili tuweze kuwajengea nyumba nzuri za kuishi hawa askari wetu wa polisi pale Makambako.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jambo lingine upande huo huo wa polisi, katika kituo chetu pale ni centre kubwa sana ya kwenda Mbeya, Songea, Liganga na kadhalika. Gari la polisi linalotumika ni la siku nyingi na wakati fulani RPC amekuwa akitoa gari kutoka Njombe. Niombe sana tuhakikishe pale tunapewa gari na wakati fulani gari lingine limechukuliwa kutoka Ludewa na ndiyo lipo pale Makambako. Kwa hiyo, niombe sana katika bajeti hii kuhakikisha tunapata gari letu la polisi ili gari la Ludewa liweze kurudi Ludewa mahali ambapo walikuwa wameliazima. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sera yetu inaelezea kujenga VETA kila Wilaya. Naomba tuhakikishe tunajenga VETA katika Wlaya yetu ya Njombe ili vijana hawa wanaomaliza darasa la saba, kidato cha nne waweze kwenda kujifunza ujuzi mbalimbali katika eneo letu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe sana Waziri wa Ujenzi, tulikuwa tumeleta maombi kupitia kikao chetu cha RCC cha Mkoa kupandisha hadhi za barabara inayotoka Makambako – Mlowa - Kifumbe - Kitandililo na barabara nyingine ya TANROAD ambayo inatoka Ikelu - Ilengititu – Kifumbe. Niombe sana kwa sababu Halmashauri haina uwezo wa kuweza kutengeneza barabara hizi tuombe zipandishwe hadhi ili kusudi ziwe zinapitika wakati wote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unajua bajeti hii hata kuchangia ni wajibu wa kuchangia lakini kama nilivyosema ni nzuri, ni lazima tuiunge mkono ili Serikali iende ikafanye kazi.
kwa sababu ya Serikali ya Awamu ya Tano na watu wanaomsaidia Rais Waheshimiwa Mawaziri, songeni mbele msisikilize maneno ya watu hawa, wanataka kuchelewesha shughuli za maendeleo. Hawa wamejipanga kuchelewesha shughuli za maendeleo ili 2020 tukwame, songeni mbele na watakwama wao. (Makofi)
Sasa umekuja hapa hutaki kuchangia na watu wamekutuma hapa uje kuchangia maana yake nini? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi niseme tu nimalizie kwa kusema naunga mkono bajeti hii naitaka Serikali kuhakikisha tunapotoka hapa inakwenda kufanya kazi zilizopangwa katika maeneo yetu, CCM!
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naunga mkono hoja.