Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja ya Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jinsi anavyotuongoza katika nchi yetu. Pia nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Afya na Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru sana Serikali kwa kuwezesha zahanati na vituo vya afya vya Jimbo la Njombe kupata dawa. Jimbo la Njombe lina changamoto nyingi za kiafya ikiwemo miundombinu, vifaa tiba, dawa na watumishi. Watumishi na wahudumu wa afya ni wachache sana. Katika Hospitali ya Kibeda Nesi moja anahudumia wagonjwa na kufanya usafi, ni kazi kubwa sana inayosababisha kushusha tija na kuleta manung’uniko kwa watumishi. Niiombe Serikali ilione suala hilo. Pia katika zahanati vijijini mhudumu akienda likizo huduma inasimama na wananchi wanakosa huduma.

Nitoe rai kwa Serikali iisaidie Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa kuiongezea watumishi wa afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Afya, lipo tatizo la tezi dume ambalo sasa linazidi kusababisha vifo vingi nchini. Niiombe Serikali iongeze nguvu katika kutoa elimu za utambuzi wa tatizo hili katika hatua za awali na tiba. Vilevile Serikali itoe elimu kwa waganga wengi ili waweze kufanya upasuaji mapema na kuepusha vifo visivyo vya lazima.