Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kuhusu fedha za Busket Fund- Mafinga Town Council. Suala hili nimelizungumzia mara kadhaa katika jitihada za kutafuta ufumbuzi. Tulitembelea TAMISEMI tukaonana na viongozi wa Wizara akiwemo NKM na Mkurugenzi wa Huduma za Afya. Ombi letu, Serikali itoe maelekezo mahsusi kwa Halmashauri Wilaya ya Mufindi sehemu ya fedha wanayopokea iende kwenye Hospitali ya Mafinga ambayo inahudumia Wilaya nzima (Mafinga TC na Mufindi DC).

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano, mwaka 2016/2017, Mafinga TC tulipangiwa shilingi milioni 101, Mufindi DC walipangiwa around shilingi milioni 700. Kwa mwongozo, inatakiwa 30% ya fedha hiyo iende ikahudumie hospitali. Kabla hatujawa Halmashauri mbili tulipokea around shilingi milioni 800 ambapo 30% yake sawa na shilingi milioni 240 ilienda kuhudumia Hospitali ya Wilaya lakini ilivyo sasa Mafinga TC tunapokea around shilingi milioni 100 ambapo 30% yake ni around shilingi milioni 30 ndiyo inayoenda kuhudumia hospitali. Kwa hiyo, utaona upungufu kutoka shilingi milioni 240 mpaka shilingi milioni 30, ni punguzo kubwa, tunapokea 12.5% tu ya kuhudumia hospitali suala ambalo linaathiri mno utendaji wa kazi na kuhatarisha maisha ya wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi letu, kwa kuwa Hospitali ya Mafinga inahudumiwa na Mafinga TC lakini function wise hospitali inahudumia Halmashauri zetu mbili, Serikali kwa maana ya Wizara ya Afya na TAMISEMI, itoe maelekezo kwa Halmashauri ya Mufindi ili sehemu ya fedha za Busket Fund zipelekwe Mafinga TC kwa nia ya kuhudumia hospitali ya Mafinga inayohudumia Wilaya nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni fedha za Mfuko wa Wanawake (5%). Nimepitia kitabu na Mafinga TC ni kati ya Halmashauri chache sana ambazo hazijawapa vikundi vya wanawake fedha zao. Hii ni kutokana na conflicting interests. Nashauri na naomba Wizara izitake Halmashauri hizo zitoe maelezo kwa nini mpaka sasa tupo robo ya mwisho ya mwaka fedha hizo hazijatolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ukiangalia katika Jedwali hata Halmashauri ambazo zimetoa fedha, percentage wise ni kasi kidogo sana. Hali hii inatokana na ukweli kwamba Halmashauri zinachukulia suala la 5% ya fedha ya Mfuko wa Wanawake kimzaha. Nitatoa mfano, kwa mujibu wa mwongozo wa matumizi ya fedha za makusanyo ya ndani 5% + 5%= 10% ni ya wanawake na vijana, 50% ya kuendeshea ofisi na 40% kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, haijawahi kutokea ile 50% ya kuendeshea ofisi ikakosekana. Halmashauri zinatumia kila kinachokusanywa kwa ajili ya kuendeshea ofisi na kupuuza kutenga fedha za Mfuko wa Wanawake. Je, Serikali imejipanga vipi katika kuhakikisha kuwa suala hili haliendelei kujirudia kwa sababu hata Kamati ya LAAC suala hili limekuwa likirudia kila mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, ni kuhusu kutoa ruzuku/ mkopo kwa wanafunzi wa kozi za uuguzi. Nimekuwa nikipendekeza kuwa kwa kuwa mahitaji ya kada hizi kuanzia AMO, Laboratory Technician na kadhalika ni makubwa na wazazi wengi wanashindwa kumudu gharama za kuwalipia, je, kwa nini Serikali isifikie hatua ikaunda utaratibu wa kutoa ruzuku/mkopo kwa wanafunzi wenye nia na sifa za kusomea fani hizo? Ahsante.