Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuwapongeza Waziri, Naibu pamoja na Watendaji wote wa Wizara kwa utendaji mzuri wa kazi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo langu ambalo nalirudia mara kwa mara katika Wizara hii ni upungufu wa Madaktari na Wauguzi katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Handeni. Hili ni tatizo kubwa sana na mara kwa mara hutokea vifo wagonjwa wakiwa wanasubiri huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilishaliongelea kwenye kipindi cha maswali na majibu, Hospitali ya Wilaya ya Handeni inahudumia takribani majimbo manne na ukiangalia hakuna bajeti yoyote ya kujenga hospitali nyingine hivi karibuni. Kutokana na hilo, hospitali inaelemewa na uhitaji wa vifaa tiba. Namwomba Mheshimiwa Waziri na kwa vile ameshatutembelea na anajua hali yetu, basi atuangalie kwa jicho la tatu kwenye vifaa tiba na madaktari. Namwomba Mheshimiwa Waziri katika majumuisho aizungumzie na Hospitali yetu ya Handeni ili hata wananchi wetu wapate imani kwamba matatizo yetu yatafanyiwa kazi.