Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Afya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Mtwara ya Mkoa haina X-Ray na iliyopo ni mbovu. Naomba kuuliza, kwa nini hospitali hii ya Mkoa wa Mtwara haipelekewi X-Ray ya uhakika wakati kila mwaka tunaongea hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali inayotumika kama ya Wilaya inaitwa Hospitali ya Likombe iliyopo Mtwara Mjini, kwa nini haina X-Ray mpaka leo? Bajeti ya mwaka 2016/ 2017 Mheshimiwa Waziri alisema hospital hizi za Mtwara Mjini zitapelekewa X-Ray, mpaka leo bado. Kwa nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Waheshimiwa Wabunge wamepewa Ambulance: kwa nini Mtwara Mjini Wizara haijatuletea Ambulance hizo? Naomba Wizara itueleze Wanamtwara Mjini, juu ya Ambulance kwa ajili ya Tarafa ya Mikindani na Tarafa ya Mjini ili kuondoa kero na adha kubwa wanayopata wagonjwa wa Mtwara Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wodi ni chache katika Hospitali ya Likombe ambayo ndiyo Hospitali ya Wilaya, Mtwara Mjini. Naomba kujua, ni lini wodi zitaongezwa, nyumba za Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Likombe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mazingira ya Wodi za Hospitali ya Mkoa (Ligula) siyo nzuri kabisa, naomba hospitali ipakwe rangi, vyoo vitengenezwe na huduma ya maji katika Hospitali ya Ligula yarekebishwe haraka iwezekanavyo, maana hali ya vyoo ni mbaya sana katika hospitali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye taarifa ya Waziri katika kitabu chake kinaonesha Mtwara Mjini dawa zinapatikana kwa asilimia 92% kitu ambacho ukienda Hospitali ya Ligula ya Mkoa na Wilaya hali ni tofauti kabisa. Wagonjwa wanaambiwa baada ya siku mbili tu dawa zimekwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ufafanuzi, kwa nini tunaambiwa dawa zinapatikana kwa asilimia kubwa, lakini hospitali dawa hakuna na zikiwepo zinakwisha kwa siku mbili tu?