Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara na Serikali kwa kujitahidi kutatua changamoto mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, hakuna mahali popote amezungumzia Hospitali ya Mkoa mpya wa Songwe. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga au kuimarisha Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, yaani Vwawa kwa kuongeza wataalam, vifaa tiba na bajeti ya hospitali ili itoe huduma kama Hospitali ya Rufaa ya Mkoa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kuhusu mahitaji ya Madaktari na Wahudumu wa Afya katika zahanati, vituo vya afya na Hospitali ya Vwawa. Hivi sasa Mhudumu wa Afya yaani (Nurse) anahudumia ward zaidi ya moja. Zahanati nyingi zimekamilika lakini zimekosa wafanyakazi, bado kufunguliwa. Suala hili linawakatisha tamaa sana wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni kuhusu umaliziaji wa majengo ya Vituo vya Afya katika sehemu mbalimbali. Madai ya muda mrefu ya stahili za Madaktari wa Wilaya ya Mbozi hususan Hospitali ya Vwawa kama vile Night Call Allowance, allowance za majukumu na kadhalika, tafadhali naomba yashughulikiwe haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muhimu; naomba maelezo ya kina, nini kinaendelea juu ya ujenzi wa Hospitali ya Mkoa wa Songwe? Hii ningependa majibu ya kina.