Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. KANYASU J. CONSTATINE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kunipatia Ambulance na pia mgawo na Madaktari wanne ambao tayari wamefika Geita. Kwa bahati mbaya mmoja bado yupo masomoni China mwaka mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba yafuatayo:-

(i) Hospitali yetu ya Wilaya imekuwa ya Rufaa ya Mkoa, kwa sasa imezidiwa sana na wagonjwa, gharama za dawa na huduma ziko juu kwa level ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa. Naomba sana juhudi za kujenga Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mheshimiwa Waziri aipe kipaumbele ili kupunguza gharama kwa wananchi.

(ii) Bado tuna uhaba mkubwa sana wa Madaktari Bingwa, Madaktari wa kati na wahudumu wa Afya, kama Nurses na watu wa Maabara. Naomba sana mwaka huu wakati wa mgao wa Watumishi wa Afya, Wizara isaidie kuitazama Hospitali ya Geita kwa jicho la huruma. Pamoja na suala hili kuwa la TAMISEMI bado Wizara ndiyo yenye jukumu.

(iii) Bado hospitali ya Rufaa ya Geita tunahitaji Duka la Dawa la MSD. Kosa kubwa limefanyika Geita ni kupeleka Duka la MSD Hospitali ya Wilaya Chato ambapo hakuna wagonjwa wengi, matokeo yake mahitaji ya msingi yamesahaulika au kupuuzwa. Ombi langu, Duka hili la Makao Makuu ya Mkoa lifunguliwe.

(iv) Ufanisi duni wa MSD, Halmashauri zetu zimekosa dawa muhimu kwenye bohari ya dawa, mafunzo yake, pesa hiyo inatumika kununua vifaa ambavyo siyo vya lazima na kuacha uhaba wa dawa ukiwa pale pale, matokeo yake MSD wanatoa O/S release kwenda kwa Private Vendor’s ambao huuza dawa na vifaa tiba kwa gharama kubwa, mara kumi zaidi ya bei ya soko ambalo watu wa kawaida wananunua. Hii maana yake ni kwamba pesa ya kutosha kutoa huduma mwezi mmoja kwa gharama za Private Vendor’s inatumika siku 10 tu.

Mheshimiwa Mwenyekti, naishauri Serikali kuhakikisha MSD wanazo dawa wakati wote kuepuka kupoteza fedha za umma.