Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika hotuba hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba Mheshimiwa Waziri akubaliane nami kuwa afya ya kiumbe hai yeyote inapotetereka na maisha yake pia yanakuwa hatarini wakati wowote. Kwa hiyo basi, afya ni kitu muhimu sana katika maisha ya mwanadamu, kiumbe hai chochote ikiwemo mimea na wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie Hospitali ya Kaloleni iliyopo Mkoa wa Arusha ambayo imekuwa ikitumika sana sehemu ya kusaidia magonjwa ya mlipuko mfano, kipindupindu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali hii haina vifaa kama dawa na hata dawa za kawaida tu za kutuliza maumivu zinashindwa kupatikana katika hospitali hii na hata karatasi za kuandikia (description) hakuna. Ukienda Nurse anakwambia kanunue daftari kwa ajili ya kuandikia. Hata dawa ya kufungia kidonda tu, hakuna. Mashuka ya kulalia na kujifunika hatuna na idadi ya mashuka hayo ni 15 tu, lakini Serikali imeshindwa kupeleka hata hii idadi ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru inafanya kazi kama siyo Hospitali ya Rufaa kwa kukosa madawa na vifaa vingi vya matibabu na naona hata Serikali ilikosea kuipa hadhi ya Hospitali ya Rufaa, kama ilikuwa haijajiandaa kupeleka vifaa hata vile muhimu tu. Achia mbali MRI, lakini ultrasound, X-Ray, hazifanyi kazi. Kuna mashine mbili za X-Ray, moja ambayo ni nzuri inaweza kufanya au kupima vipimo vingi, haifanyi kazi kwa muda mrefu sasa na inayofanya kazi ni moja tu, ambayo haipimi vitu vingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Serikali iangalie hospitali hii na kuitendea haki kama Hospitali ya Rufaa.