Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri yenye mwelekeo wa kuboresha afya ya Watanzania. Pia nawapongeza Naibu Waziri na Katibu Mkuu na Watumishi wote wa Wizara kwa kujituma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado utoaji huduma ya afya katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ni changamoto kubwa. Hospitali hii ni ya zamani sana tangu uhuru, miundombinu ya hospitali ni chakavu sana na haitoshi. Hospitali inahitaji wodi za wanawake, wodi za wanaume, chumba cha kujifungulia, wodi ya wazazi, OPD na miundombinu mingine. OPD kwa mfano, ni chakavu sana, inahitaji ujenzi mpya. Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo haina uwezo wa kugharamia ujenzi na ukarabati mkubwa unaohitajika. Namwomba Mheshimiwa Waziri aiwezeshe Halmashauri kwa bajeti maalum ili kuiboresha hospitali hii iweze kutoa huduma bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiacha upungufu wa miundombinu, hospitali ya Wilaya pia ina upungufu wa vifaa tiba na madawa. Nashauri Wizara itusimamie katika matatizo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.