Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia mpango wa uzazi. Rejea hotuba ya Mheshimiwa Waziri Ibara ya 43, ukurasa wa 16, nitanukuu mwisho wa Ibara hiyo: “Wizara kwa kushirikiana na wadau, imetoa mafunzo kwa watoa huduma 3,233 ili kuwajengea uwezo wa kutoa huduma za aina mbalimbali za uzazi wa mpango. Hadi sasa kiwango cha kutumia uzazi wa mpango kimepanda kutoka asilimia 27 mwaka 2010 hadi asilimia 32 mwaka 2015/2016. Lengo ni kufikia asilimia 45 mwaka 2020.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii kasi ni ndogo sana. Ajenda ya mpango wa uzazi inahitaji kupewa kipaumbele kama mkakati sahihi wa kukabiliana na changamoto zetu za maendeleo. Tanzania ina kasi ya asilimia 2.9 ya ongezeko la watu, kasi ambayo ni kubwa. Akinamama wengi huzaa
wastani wa watoto watano. Idadi ya watu inakadiriwa kufikia milioni 65 ifikapo mwaka 2025, miaka nane kutoka sasa. Idadi kubwa ya watu ina matokeo hasi kwa maendeleo, ukuaji wa Miji na maisha ya watu (socio- economic growth); inagusa malengo yetu ya maendeleo endelevu katika sekta karibu zote; elimu, afya, uchumi, kilimo, mazingira na Miji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kasi ya kuzaliana ikipungua tutakuwa na rasilimali za kutosha kuboresha elimu na kilimo chetu. Elimu na kilimo ni sekta muhimu kwa nchi yetu, idadi ikipungua, Serikali itaweza kuweka akiba na kuongeza uwekezaji kukuza uchumi wetu, ujenzi wa reli, barabara, bandari, viwanja vya ndege na kadhalika, zikiwemo shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara hii ipatiwe bajeti ya kutosha kuwezesha Halmashauri kutekeleza mipango ya uzazi (family planning) yenye matokeo. Programme za afya ya mama na mtoto zipewe uzito stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.