Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa kibali cha kuchangia hotuba ya bajeti ya Wizara hii kimaandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mawaziri wa Wizara hii, Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Mheshimiwa Dkt. Hamis Kigwangalla kwa kazi nzuri ya kusimamia mapinduzi makubwa ya uboreshaji wa huduma za afya nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi zinajieleza kwenye maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko la bajeti ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2015/ 2016 mpaka shilingi bilioni 251.5 kwa mwaka huu 2016/2017. Utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/2017 imetoa matumaini makubwa ambapo mpaka sasa kiasi cha shilingi bilioni 112.19 zilipokelewa MSD. Kati ya hizo, Mkoa wa Pwani Hospitali zetu na Vituo vya Afya tunategemea kiasi cha shilingi bilioni 1.6. Tunawapongeza sana kwa jitihada hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ununuzi na usambazaji wa vitanda vya kawaida 20, vitanda vya kujifungulia vitano, magodoro 25 na mashuka 50 kwa Halmashauri zetu zote vilivyogharimu shilingi bilioni 2.93.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mfuko wa Bima ya Afya ya Pamoja, napongeza hatua zilizochukuliwa na Wizara kuhakikisha kuwa fedha za dawa kupitia Mfuko wa Pamoja zitapelekwa moja kwa moja kwenye vituo vya kutolea huduma, hatua hii itachangia upatikanaji dawa kwa wakati kwa wananchi wetu. Pamoja na pongezi hizo, katika maeneo machache naomba kushauri yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Halmashauri yetu ya Chalinze, Wizara ilikubali ombi la kupandisha hadhi Kituo cha Afya Msoga kuwa Hospitali ya Halmashauri. Ombi langu, naomba Wizara ilete watumishi ili kukidhi haja ya kuipandisha hadhi. Kukosekana kwa watumishi wa Sekta ya Afya katika Hospitali hiyo tarajiwa ya Halmashauri, imepelekea pesa za Basket Fund takriban shilingi milioni 90 kati ya fedha zote zilizopokelewa kushindwa kutumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kusimamia ahadi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne ya kupandisha hadhi Kituo cha Afya Mlandizi kuwa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Vijijini na Kituo cha Afya Kibiti kuwa Hospitali ya Wilaya mpya ya Kibiti. Maeneo haya yana wananchi wengi, hivyo vituo hivyo vinazidiwa na idadi ya wagonjwa, lakini kuwa na mgawo ule ule wa hadhi ya kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.