Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Afya, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote, nianze kwa kuwapongeza kwa kazi nzuri ya kuwahudumia Watanzania. Binafsi ninawashukuru sana Waziri na Naibu Waziri kwa ushirikiano mnaonipa kuwahudumia wananchi wa Jimbo la Karagwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maombi mawili ambayo ni kwanza kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Hatua za awali kwenye Halmashauri na RCC zimekamilika tunakwamishwa na urasimu, ipo kwenye mchakato kwa upande wa Serikali Kuu. Wizara ya Ujenzi tayari imeridhia majengo ya TANROADS yaliyopo karibu na Makao Makuu ya Wilaya eneo la Kihanga yatumiwe kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya. Tunaishukuru sana Wizara ya Ujenzi.

Naiomba Wizara ya Afya uwapanguse machozi wananchi wa Karagwe kwa kushirikiana na TAMISEMI ili kiasi cha fedha kitengwe kwenye bajeti mwaka 2017/2018 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali, hata kama ni kiasi kidogo cha fedha. Nitashika shilingi ya Waziri iwapo sitapata maelezo ya kuridhisha juu ya jambo hili. TANROADS itachukua majengo yake iwapo ujenzi wa hospitali hautaanza mwaka 2017/2018 kama tulivyoahidiwa kwenye maombi yetu na ombi namba mbili, please refer to request number one.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.