Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia Wizara hii, kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara hii kwa uwajibikaji wao mzuri, hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ni ukosefu wa magari ya wagonjwa katika Jimbo langu la Kwela na hasa kituo cha afya Milepa, kituo ambacho kiko mbali na huduma na kiko katika mazingira magumu na kinaongoza kwa vifo vya akina mama wajawazito na watoto. Naomba kujua kwa nini Serikali haitaki kupeleka gari, kuna nini? Tunajua wazi yapo maeneo yanagawiwa magari karibu vituo vyote vya afya walivyonavyo. Mheshimiwa Waziri mnatumia vigezo gani? Nimesema tatizo la gari katika kituo hiki toka mwaka 2012 bado sijafanikiwa.

Naomba nijibiwe hii siyo haki, baadae natarajia, kutoa idadi ya vifo vya akina mama na watoto waliopoteza maisha yao kwa kungojelea gari la wagonjwa hadi kufa kwa kukosa msaada wa gari la wagonjwa.