Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niwapongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa hotuba nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Wizara/Serikali kuangalia uwezekano wa kuziongezea fedha programu za NACP/NBTS/NTLP kwa kuwa ufadhili wa PEPFAR/CDC umepungua sana. Serikali iangalie uwezekano wa kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha ofisi ijulikanayo kama mradi wa NACP/NTLP Joint Office Project iliyopo nyuma ya ofisi za WHO. Mradi huu ulisimama miaka mingi iliyopita kufuatia Global Fund kuacha kutoa fedha kwa ajili ya jengo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali ya Wilaya ya Mbinga tunaomba kuboreshewa huduma za upasuaji. Vilevile kwa kadri hali itakavyowezekana tunaomba hospitali hii ipatiwe chumba cha kuhifadhi maiti (mortuary).

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Wizara iangalie uwezekano wa kukipandisha Kituo cha Afya cha Mapera ili kiweze kuhudumia kama Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga baada ya kuipandisha hadhi ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaipongeza Serikali kwa kugawa vifaa tiba kwa kila Halmashauri. Ushauri wangu ni kwamba vifaa hivyo vigawiwe kupitia Mbunge kama ilivyofanyika kwenye mgao wa madawati ya chenji ya Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.