Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Wizara hii, ninaomba vitu viwili:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kilolo ni kati ya Wilaya kubwa Tanzania, ilianzishwa mwaka 2002 lakini hatuna Hospitali ya Wilaya na kituo cha afya ni kimoja tu. Ili mwananchi apate matibabu inabidi asafiri kilometa 100 hadi Ilula. Changamoto kubwa ni gari la wagonjwa, yaani gari langu sasa limekuwa gari la wagonjwa; Mheshimiwa Naibu Waziri anajua sana tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ninaomba sana nipate gari Wilaya ya Kilolo. Bado tuna ikama kubwa ya watumishi wa afya. Tunaomba sana uwasiliane na Wizara ya Utumishi ili tuongezewe watumishi.