Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza kabisa nishukuru katika Jimbo langu la Bunda kituo cha afya cha Manyamanyama tumepata gari la kubebea wagonjwa, ahsante sana; lakini katika yote usisahau kinahitaji kupandishwa hadhi. Imemshinda mama Anna Abdalah, Mwakyusa na ni sasa ndugu yangu Kigwangalla na Mheshimiwa Ummy dada angu mbali na kazi zote anazozifanya Manyamanyama tunahitaji iwe hospitali ya Wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, tumekuwa tukizungumza humu ndani tutamsulubu Ummy, tutamsulubu Kigwangalla, lakini wote tunatakiwa tuibane Serikali itimize, Azimio la Abuja la kutenga asilimia 15 ya bajeti ya Serikali Kuu iende kwenye Sekta ya Afya. Hawa hata kama wawe na misuli ya kufanya kazi kiasi gani wasipopewa fedha, hawawezi kutimiza majukumu yao.

Mheshimiwa Menyekiti, hilo ndilo jambo la ukweli lazima tuseme, asilimia 15 na hapa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha upo na wewe na mama unalisikia hilo, lazima uhakikishe Azimio la Abuja na Tanzania tumesaini linatekelezwa, kwa sababu zikitengwa asilimia 15 angalau changamoto ya Sekta ya Afya nchini itapungua na imekuwa ni kubwa; kuna tatizo la madawa, kuna kansa ya uzazi, kuna matatizo ya ugonjwa wa akili ambayo yamesahaulika kabisa. Yote hayo hayawezi yakafanikiwa kama tusipotimiza lile Azimio la Abuja la kutenga asilimia 15 kwenye bajeti kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nchi za wenzetu South Africa, Zambia, kuna mambo ambayo wameyafanya, fedha za dawa na vifaa tiba zinatokana na matumizi ya kawaida, ambazo ni fedha ndani, ni Bunge hili sisi kuamua, taratibu siyo misaafu, tukihakikisha pesa za dawa tunaziweka katika fungu la matumizi ya kawaida, uhakika wa fedha zetu za ndani kwenda katika madawa na vifaa tiba utakuwa mkubwa. Hapa nimpongeze mdogo wangu Upendo Peneza, aliomba kuleta hoja binafsi katika Bunge hili Tukufu lakini hakupata nafasi. Kwa hiyo lazima tubadilishe utaratibu na sisi si wa kwanza, tukifanya hivyo, si tu tutakuwa tumetatua changamoto katika sekta ya afya, tutakuwa tumeokoa vifo vya akinamama na watoto na tutakuwa tumetatua matatizo mengi ambayo yapo katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine Mheshimiwa Waziri Vyuo vya Maendeleo ya Jamii. Kabla Wizara hii haijaunganishwa unakijua Chuo cha Kisangwa Bunda kina matatizo lukuki. Naomba chuo hicho mhakikishe kinapewa fedha za kutosha ili kutatua matatizo yaliyopo. Kingine gari ambalo limechukuliwa kinyume na taratibu, Wizara ilishaagiza gari lile lirudishwe, aliyekuwa Mkuu wa Chuo alijiuzia kinyume na utaratibu na barua ziko Wizarani, hakuna shangingi linalouzwa kwa shilingi laki tano, niliwaambia, naomba wizi huo mimi Jimboni marufuku sitaki nimeshaanza kusafisha. Kama ulikuwa kipindi hicho cha nyuma nimeshaingia mimi, sitaki biashara ya wizi Jimbo la Bunda, ni maendeleo tu. Naomba mambo hayo yote yazingatiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri na ndugu yangu Dkt. Kingwangalla, yeye ni Daktari na tulikuwa wote, back benchers huko. Suala la tatizo la afya ya akili pale Muhimbili, kila siku kati ya wagonjwa 150 mpaka 200 wanaenda pale, zile dawa ni ghali, sasa hivi wanachangia. Ukiangalia moja ya matatizo hayo yapo kwenye kurithi na yanachangia umaskini mkubwa, lakini kitengo hiki kimesahaulika kabisa. Mimi si daktari lakini wanasema matatizo yale kuna stage, lakini sometimes mgonjwa anaruhusiwa kwenda kwa sababu tu hakuna vitanda, hakuna maeneo ya kutosha ya kuwahifadhi wale. Kwa hiyo naomba mlifanyie kazi sana, tuwape…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)