Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwnyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwashukuru Waziri na Naibu wake na watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya. Niendelee kutoa pongezi kwa Jemedari wetu, Rais wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayofanya, sina mashaka na yeye. Wasiwasi wangu ni kwamba akimaliza miaka yake kumi atakuja mtu mzuri kama yeye au vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Hospitali ya Mkoa wa Mara. Sijajua kwa Mkoa wetu wa Mara ni kitu gani kinatokea kwa sababu vitu vingi haviendi vizuri. Hospitali hii imechangiwa karibu miaka 32 na haijaisha. Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara ya Kongwa, imekuwa ikitengewa fedha kidogo kila mwaka na mpaka leo haijulikani itaisha lini. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri anapokuja hapa atueleza kwa mwaka huu wa fedha imetengewa kiasi gani na ni lini hospitali inaweza kwisha? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba ya Waziri, nadhani ukurasa wa 149, anazungumzia habari ya kupeleka fedha za vijana na akina mama katika vikundi. Katika Wilaya ya Bunda wameandika kwamba imepeleka shilingi milioni 106, nikashangaa! Sasa nataka kujiuliza haya maandishi humu ni ya kweli au mtu ameyabandika tu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, asubuhi nimempigia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kumuuliza hii hela mmepeleka ninyi? Anasema sisi tumepeleka shilingi milioni 20 tu. Maana Bunda yenyewe kukusanya shilingi milioni 100 ni kesi. Sasa nataka kujiuliza hizi fedha zimetoka Wizarani za muda mrefu au za namna gani? Kwa hiyo, kama ni za Wizarani ni sawa lakini kama ni za kutoka kwenye Halmashauri na ni own source, hizi fedha hazijatoka. Kwa hiyo, nataka kuuliza suala hili limekaaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine nizungumzie habari ya watumishi katika Jimbo langu la Bunda. Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla ametembelea katika Jimbo langu la Bunda ameona katika kila kituo nurse ni mmoja-mmoja tena wale wa daraja la chini na akaahidi mtakapopata nafasi mtatuletea watumishi katika Jimbo la Bunda. Zahanati zote zina nurse mmoja-mmoja na Naibu Waziri ameshuhudia mwenyewe. Kwa hiyo, naomba katika nafasi zitakazopatikana mnisaidie kupata watumishi wa maeneo hayo. (Makofi)

Lakini pia mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma za Jamii. Tumetembelea Muhimbili, Ocean Road na maeneo mengine mengi, fedha haziendi kwenye vituo vyote vikuu. Tunaiomba Serikali katika bajeti inazotenga fedha ziende kwenye maeneo muhimu ambayo imezitengea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tumeona Mloganzila, tumeambiwa kile Kituo cha Ufundishaji cha Tiba kimeisha lakini hakina watumishi. Kinahitaji fedha kiasi cha shilingi bilioni nne ili kianze kazi. Tunaomba Serikali ipeleke pale madaktari na kituo kile kiweze kuanza kazi mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna Hospitali yetu ya Benjamin Mkapa iko hapa, tunaomba watumishi waende maeneo hayo ili waweze kusaidia wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna Hospitali ya Nyamuswa, ni kituo ambacho tumekijenga kiko kwenye hali nzuri. Tunaomba pale mtakapopata x-ray na nimesikia Waziri anasema mtapata x-ray basi mtupelekee kwenye Kituo cya Nyamuswa ili watu waweze kupata huduma katika maeneo yale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia katika haya mambo ya vijana mimi nadhani sasa kuwepo na mkakati maalum kupitia hii Wizara na Wizara ya Kazi tujue sasa hizi fedha za taasisi za kijamii zinazoenda kwa ajili ya kuwakopesha akina mama na vijana zina mfumo mzuri ambao unaeleweka. Maana inaonekana kwamba kuna maeneo mengine yanapata fedha kutoka makao makuu na wengine wanapata kutoka own source sasa haijulikani ni wapi wanapata manufaa. Nashauri tuweke mfuko mmoja wa hizi fedha zijulikane kwamba…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda wako umekwisha.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.