Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru nianze kabisa kwa kuunga mkono hoja.

Mimi nina mambo machache, jambo la kwanza alilisema Mheshimiwa Selemani Zedi, tarehe 19 Januari, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega alimuandikia Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kuitaka kampuni inayoitwa Mokasi Medical Systems and Electronics iliyopewa mkataba wa ku-service x-ray waje waifanyie marekebisho x-ray ya Hospitali ya Wilaya ya Nzega. Mpaka leo ni miezi mitano, ninataka nimuombe Mheshimiwa Waziri anapokuja ku-wind up atuambie kwa nini, kwa sababu nimemsikia hata ndugu yangu wa Mafia amelalamika sana kuhusu hili suala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini hii kampuni kama ina mkataba na Serikali usivunjwe huu mkataba? Jambo la kwanza. Jambo la pili kwa nini hatua za kisheria zisichukuliwe? Hili ni jambo ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega na Halmashauri ya Mji wa Nzega wanapata shida, x-ray ipo, hairuhusiwi kuguswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe taarifa kwenye Bunge na nimpongeze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, ninaamini kaka yangu Simbachawene hatamchukulia hatua kwa maamuzi aliyoyafanya huyu Mkurugenzi. Mkurugenzi ameamua kuwasialiana na Hospitali ya Rufaa kwa ajili ya kumpata Biomedical Engineer anaitwa Emmanuel Nkusi kutoka Bugando ili aje aweze kwa sababu ni mtaalamu kushughulikia suala la x-ray ya Hospitali ya Wilaya ya Nzega. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kwamba kwa kuwa mkataba ni Philips huyu mtu amefanya maamuzi kwa kuangalia maslaha mapana ya nchi, nataka niseme kwamba maamuzi haya yamefanyika na mtaalamu amefika na ameshalipwa na amechukua kifaa kuondoka nacho. (Makofi)

Hoja yangu, Mheshimiwa Waziri anapokuja why huyu Mokasi asifukuzwe kufanya hizi kazi, hili ni jambo moja. Jambo la pili mimi ni mpongeze sana Mheshimiwa Rais, mimi ni mjumbe wa Kamati, support aliyoitoa Mheshimiwa Rais kwenye suala la hospitali ya Ocean Road na tunafahamu matatizo ya cancer, na mimi nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Ummy kwa sababu tupo kwenye Kamati yeye na Mheshimiwa Kigwangalla tunaona tatizo la resource lililopo na namna anavyoweka priority, nataka niombe kwa ushauri, mwaka huu tunamaliza ile Phase II pale Ocean Road na tutakuwa kwenye nafasi nzuri sana kwenye Ocean Road. Niombe jitihada ziongezwe kwenye Hospitali ya Kikwete ya Moyo na Hospitali ya MOI ili ziweze kuongeza utoaji wa huduma katika maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho nataka niishauri Serikali, Ilani yetu ya uchaguzi it is very clear, kwamba kila kijiji - zahanati na kila kata - kituo cha afya, hii ndiyo commentment yetu kwa Watanzania. Ningeomba kuwepo na proper plan na kuwe kuna strategic unit kati ya Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Afya ni namna gani tunajenga kila mwaka vituo vya afya. Kama kila Halmashauri ikiwekewa condition kwamba kila mwaka wa fedha angalau vijengwe vituo viwili, vitatu vya afya tuna uwezo wa kupata kwa mwaka angalau vituo 200 vya afya. Hii itatusaidia sana kupunguza matatizo katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niwapongeze sana Wizara ya Afya na TAMISEMI, kuwepo kwa Dkt. Chaula pale anayeshughulika na masuala ya afya, angalau anatupunguzia.

Nataka niwaombe Mheshimiwa Simbachawene na Waziri wa Afya, hebu ondoeni haka ka-condition kwa tofauli za nchi sita. Kule kwenye Halmashauri wananchi tumewahamasisha, mfano kwangu sasa hivi tunavyoongea tuna zahanati 15 tunajenga sisi wananchi, zimefika kwenye level ya madirisha, lakini kuna kale ile condition ya kusema kwamba ili ujenge zahanati lazima iwe tofali ya nchi sita. Tofali ya nchi sita kwa kule kwetu Nzega ni 1200, mwaka huu mimi nimegawa matofali 47,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukichukua hiyo twenty percent ya incremental cost ni milioni tisa na laki nne, gharama additional cost. Hivyo, tuwe na flexibility kwenye haya mambo ili angalau kama tulivyojenga madarasa katika kuanzishwa kwa shule za kata, wananchi walijitahidi sana kwa sababu tuliondoa zile condition za ki-engineer. Niombe sana Serikali iangalie namna gani Serikali inaweza kufanya jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuwapongeza kwa jitihada mnazofanya lakini Mheshimiwa Waziri usipokuja na hoja ya huyu Mokasi Medical Systems.....

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: ….nitashika shilingi. Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti.