Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa utendaji wake wa kazi. Mwenyezi Mungu aendelee, kumpatia afya njema, aendelea kuimarisha Tanzania yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu Ndugu Nyamhanga na Watendaji wote wanaofanya kazi katika Wizara hii, hongereni sana na endeleeni kuchapa kazi tupo pamoja nanyi na kazi yenu Watanzania wanatambua uwezo wenu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waziri na Katibu wa Wizara hii Ndugu, Nyamhanga, kwa kusikiliza kilio cha wananchi wa Jimbo langu la Kwela, kilio cha muda mrefu, juu ya barabara sugu na yenye gharama kubwa ambayo Halmashauri haina uwezo nayo kwa maombi yangu. Kwanza ulitupatia milioni 431 na bado barabara hiyo ichukuliwe na TANROAD. Nashukuru barabara hiyo leo imekwishachukuliwa na TANROAD. Ahsante sana na Mwenyezi Mungu awabariki katika kazi zenu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru vilevile kwa kuanza utaratibu wa ujenzi wa daraja la Mto Momba. Daraja ambalo ni kiungo kikubwa kwa barabara ya Kibaoni - Kulyamatundu, Kamsamba, Mlowo, tunaomba kasi iendelee katika kuanza kulijenga Daraja hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali iharakishe kufanya usanifu katika barabara ya Kibaoni, Kilyamatundu, Kamsamba, Mlowo. Barabara hii ni muhimu sana kiuchumi kutokana uzalishaji wa mazao ya mpunga, mbaazi, matunda mbalimbali, samaki na mifugo. Tunaomba barabara hii itengenezwe haraka kwa kiwango cha lami ili kusaidia wananchi katika ukanda huo wa bonde la Ziwa Rukwa.

Maombi ya fedha kwa barabara ambazo Halmashauri haina uwezo nazo ambazo ni barabara ya Miangalua - Chombe - Kipeta, barabara ya Mawenzusi - Msia, barabara ya Mlimani inayounganisha Bonde la Rukwa na Sumbawanga kilomita 47. Pia maombi ya fedha ili kutengeneza daraja la Kaengesa, daraja la Laela kwenda Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.