Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi; katika Mkoa wa Dar es Salaam na hasa Jimbo la Ukonga kuna mnada wa Kimataifa wa Pugu. Barabara ya kwenda mnadani ni mbovu na mwaka 2016/2017 ilipangwa kujengwa lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika, naomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana azingatie barabara hii muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Ukonga kuna shida ya mawasiliano hasa Kata za Msongola, Zingiriwa, Chanika, Kivule, Mzinga, Buyuni, Pugu, Pugu Station na Majohe, je, kwa nini Mheshimiwa Waziri asihimize uwekaji wa mitandao ya simu ili Kata hizo zipate mawasiliano ya uhakika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna malalamiko mengi ya wananchi waliohamishwa kutoka Kipawa na kupelekwa Buyuni, Zavala na Kipawa Mpya. Naomba kujua mipango ya Serikali kulipa fidia wahanga na kupeleka miundombinu kama walivyokubaliana na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.