Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

HE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali na Wizara ituambie ni kwa muda gani wale nyumba zao zilizopigwa (X) zilizopo au zilizokutwa na sheria ya mwaka 2007 zitafidiwa kwa kuwa sasa hawaruhusiwi kabisa kufanya maendeleo yoyote. Ni vyema wakaruhusiwa kufanya ukarabati not ujenzi wa nyumba hizo kwa kuwa hata zikidondoka kwa sasa hawaruhusiwi kukarabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ng’ombe, punda wanachungwa pembezoni mwa barabara wanasababisha sana ajali, hivyo TANROADS kote nchini watakiwe kuweka doria kwa wanaochunga ng’ombe, punda, mbuzi, kondoo pembezoni ya barabara wachukuliwe hatua kali sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, minara ya simu kwenye vijiji vyenye kuwa na tatizo la mawasiliano wasaidiwe upesi kama vile vilivyopo Babati. Mfano, Himiti, Chemchem, Imbilili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgao wa fedha za Mfuko wa Barabara TANROAD; asilimia 70 za fedha za Mfuko wa Barabara upunguzwe hadi asilimia 50 ili wananchi wa Tasime wenye barabara nyingi wasaidiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, all the best brothers.