Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naipongeza Wizara, Waziri na Naibu Waziri wake pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara, pia nampongeza Mkurugenzi Mkuu wa Bandari kwa jitihada yake binafsi kwa kutangaza tenda ya kujenga Bandari ya Kabwe mwaka huu, pia kwa kujenga barabara ya kwenda kwenye Bandari ya Kipili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu maalum ni kuhusu mtandao wa simu katika Kata nzima ya Korongwe. Kata hii ya Korongwe haina kabisa mtandao wa simu wa aina yoyote ile, imekuwa ombi langu kubwa sana na mara kwa mara ombi hilo nazungumza moja kwa moja na Mheshimiwa Waziri Mbarawa na kweli anafanya jitihada kubwa sana kuzungumza na jamaa wa Halotel lakini mpaka leo hawajatekeleza na hata dalili hakuna kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna ombi la Mkoa wa Rukwa kuhusu barabara ya Namanyere-Kirando kuweka kwa kiwango cha lami kwa kuwa RCC Rukwa walikwisha pendekeza na kutuma maombi barabara hiyo ya kilometa 64 ijengwe kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Marine Service (MSCL) wafanyakazi wake karibu wote hawajapata mishahara yao, Wizara ifikirie sana kuhusu MSCL hailipi kabisa, mishahara ya wafanyakazi mfano, wafanyakazi wa MV Liemba muda wa miezi 13 hawajalipwa chochote, je wataishi vipi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu bandari ya Kirando iliyopo Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa, kuna mtumishi wa TPA hapo wa kuchukua ushuru wa mizigo inayopitia hapo katika kijiji hicho. TPA hawajaweka huduma yoyote ile katika kijiji hicho kilichopo kando ya Ziwa Tanganyika. Kwa kuwa, wafanyabiashara wengi wanapitia hapo nashauri sana TPA kujenga bandari ndogo ya maboti katika Kijiji hicho cha Kirando.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nategemea Mkurugenzi wa bandari atalifanyia kazi suala hilo ili kutoa malalamiko ya wafanyabiashara kulipia wakati hakuna huduma kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.