Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

HE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kutoa pongezi kwa Wizara kufanya kazi nzuri hadi sasa, napenda kuzungumzia barabara zifuatazo ambazo zimekuwa zikiombewa fedha kwa Serikali Kuu katika kuongeza nguvu kwenye Halmashauri kuzifanyia kazi pasipo na mafanikio:-
(i) Kitosi – Wampembe – kilometa 68, imepewa shilingi milioni 84 ambazo ni pungufu na fedha za 2016/2017 ni dhahiri kwa barabara hii hazikidhi mahitaji na ndio maana kuna maombi ya kuchukuliwa na TANROAD.
(ii) Nkana – Kala – kilomita 67, kijiografia Halmashauri haiwezi kuifanyia huduma katika ukamilifu wake. Serikali Kuu ni vema kuiangilia vinginevyo kwa maslahi ya wananchi wetu.
(iii) Namanyere – Ninde – kilomita 40, imekuwa ni barabara yenye maombi maalum kila mara, hii ya milioni 350 haijakamilishwa na barabara haijakamilika, hivyo Kata ya Kala haijafunguka. Tunaomba kuongezewa fedha ambazo zitakamilisha barabara hii kwa sasa.
(iv) Kasu – Katani – Miyula – kilomita 24, Mkoa wa Rukwa ni mzalishaji mkubwa wa mazao ya nafaka kwa chakula na biashara na wahusika zaidi ni akinamama na vijana wao. Barabara hii imekuwa ni mzigo mzito kwa Halmashauri na kuwa kero kwa wananchi wetu kutowawezesha kufika kwenye soko na kusababisha mazao kuharibika. Tunaomba Serikali Kuu kuwawezesha kiwango fulani Halmashauri ya Nkasi kuweza kuimarisha barabara hiyo kwa kunusurisha vifo kwa akinamama kufuata huduma ya afya. Kuwainua wananchi kiuchumi, kuwarahisishia kufika kwenye soko kwa uharaka zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri; kwa kuwa kila Mbunge anazungumzia kupandishwa kwa barabara zao na kwenda chini ya TANROAD na Serikali kuona Bodi ya Wakala ya Barabara Vijijini kuanzishwa kwa tatizo hili. Naomba kutoa ushauri wangu kuwa kutokana na kazi zenye tija kubwa na uimara wake ni vema:-
- TANROAD ikaongezewa fedha kutoka bilioni 30 kutokana na kazi kubwa wanayofanya.
- Vema TANROAD kuongezewa rasilimali watu na rasilimali fedha, kwa kuzingatia kuwa huduma zao zitalazimika kufika hadi barabara za vijijini (barabara zote zilizopo hapa nchini) hakuna sababu ya kuanzisha Bodi ya Wakala wa Barabara Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano; napenda kuzungumzia Kata ya Kala kwa ujumla wake ndani ya Vijiji vya King’ombe, Mlambo, Kapumpuli, Mpasa, Kilambo, Lolesha, Kala na Tundu.
- Hawana mawasiliano ya simu na barabara.
- Eneo hili ni mpakani mwa nchi yetu na DRC – Congo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kuona umuhimu wa kushauri na kuelekeza kampuni kadhaa maeneo hayo, nao wapate mawasiliano ya simu, ukizingatia usalama kwa wananchi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na kazi nzuri inayofanywa na Wizara hii, bali bajeti inakuwa finyu na kutokana na umuhimu na uharaka wa maendeleo haya kwenye Mkoa wa Rukwa ndiyo maana tunaomba Wizara kuongezewa fedha na miradi husika kukamilika ndani ya muda mfupi na kwa kiwango cha kudumu muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Serikali kutenga fedha za matengenezo ya barabara kwa kiwango cha changarawe na udongo zipatazo shilingi 1,350,906,000.
(i) Ntendo – Muze – kilomita 8, shilingi milioni 249,245
(ii) Muze – Mtowisa – kilomita 7, shilingi milioni 218,089
(iii) Mtowisa – Ilemba – kilomita 20 shilingi milioni 623,111
(iv) Ilemba – Kaoze – kilomita 8.36 shilingi milioni 260,461
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi ni maeneo ya ndani ya barabara ya Kibaoni – Muze – Mtowisa – Ilemba – Kaoze – Kilyamatundu – Kamsamba – Mlowo, ambayo inaunganisha Mikoa ya Katavi – Rukwa – Songwe. Kwa azma ya Serikali ya kuunganisha mikoa hapa nchini. Naomba sasa ijipange kwa kuitoa barabara hii kwenye bajeti ya kuitengeneza kwa kiwango cha changarawe na udongo na kuiweka kwenye fungu la barabara za kiwango cha lami ili mikoa hii iweze kuunganishwa.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kiwanja cha ndege Sumbawanga. Nashukuru kwa kutengewa fedha milioni 18,400. Tunachoomba ni ukamilifu wa malipo ya fidia ya wananchi wanaotoa majengo yao kuachia upanuzi wa kiwanja hicho kwa wakati na thamani ya fedha zao kwa sasa. Tunaomba usimamizi wa ujenzi huo kuwa wa karibu zaidi na kukamilika mapema kwa kiwango takiwa ili wananchi wa Rukwa waondokane na usumbufu na adha kadhaa za kukimbilia Songwe Airport.
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.